Picha: wikipedia
Asante Rais wa Benki ya Dunia Bwana Jim Yong Kim kwa kuiamini nchi yetu Tanzania. Haya yametokana na maneno yake katika uzinduzi wa ujenzi wa barabara za juu na chini (ubungo interchange) jumatatu 20 Machi 2017 jijini Dar es Salaam. Pia Rais huyu wa Benki ya Dunia amefurahia utendaji wa Rais wa Tanzania Mh Dkt John Pombe Magufuli hasa katika mapambano dhidi ya rushwa na kuleta maendeleo nchini.
Hii ni ishara kuwa Rais wa Tanzania na uongozi wake unachapa kazi kwa ajili ya maendeleo ya watanzania. Watanzania tuwe kitu kimoja katika kuiletea nchi hii maendeleo ya kweli.
No comments:
Post a Comment