Tuesday, June 6, 2017

Hongera mama Anna Mghwira kwa kuchaguliwa na rais kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro

Image may contain: 8 people, people smiling, people standing and suit

Hongera mama Anna Mghwira kwa kuchaguliwa na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKT John Pombe Magufuli. Blogu hii inakutakia kila la kheri katika utendaji wako mpya wa Ukuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Ingizo lako katika serikali ni shule kwa watanzania wote, wenye vyama na wasio na vyama. Blogu hii inakuomba uwe mfano katika uwajibikaji kwa rais na kwa wananchi, hasa wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro, uwe mwadilifu, mchapakazi na mtetea usawa kwa wote na hasa kwa kina mama na wanawake ambao bado katika nchi za kiafrika wanakabiliwa na changamoto nyingi. Aidha blogu hii inampongeza sana Mh Rais kwa uamuzi wake wa kumwamini mama ANNA ambaye awali alikuwa mwenyekiti wa chama cha upinzani ACT Wazalendo. 

No comments:

Post a Comment