Wednesday, September 25, 2013

Hongera serikali ya Tanzania kwa kusaini mkataba wa ushirikiano wa serikali zinazoendeshwa kwa uwazi DUNIANI

Hongera serikali ya Tanzania kwa kusaini mkataba wa ushirikiano wa serikali zinazoendeshwa kwa uwazi duniani. Hakika hatua hii ni nzuri kwa ustawi wa taifa lolote hasa Tanzania. Nchi nyingi zimepiga hatua ya maendeleo kwa kuwa na uwazi pamoja na utawala bora. Hivi karibuni Rais Obama wa Marekani ameipongeza Tanzania kwa kusaini mkataba huo. Blogu hii inatoa pongezi za dhati kwa serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na hasa kwa Mh. Rais Jakaya Kikwete kwa kutambua umuhimu wa uwazi katika maendeleo nchini. MUNGU IBARIKI TANZANIA! Chanzo: Habari Leo

Picha: umuseke

No comments:

Post a Comment