Thursday, November 5, 2015

Hongera Mh MAGUFULI kwa kuapishwa na kuwa Rais wa TANZANIA

Picha:taarifa.co.tz

Hongera Mh. DKT. John Pombe MAGUFULI kwa kuapishwa na kuwa Rais wa awamu ya 5 ya Tanzania. Leo alhamisi tarehe 05 Novemba 2015 ni siku ya kukumbukwa na watanzania mara baada ya kuapishwa kama Rais wa Tanzania. Hakika watanzania wamekuamini na wanakutegemea katika kuwaletea maendeleo ya kweli. Ni matumaini ya Blogu hii kuwa utawaletea watanzania maendeleo kwa kasi kubwa. Blogu hii inaamini imepata mtetezi wa wanyonge. Mwenyezi MUNGU akubariki na kukulinda katika kuwatumikia wananchi wote.

Aidha Blogu hii inawaomba watanzania wote waunganishe NGUVU katika kuhakikisha ahadi za MAGUFULI na CCM zinatekelezwa kikamilifu. 

No comments:

Post a Comment