Wednesday, November 18, 2015

Hongera Mh Ndugai kwa kuchaguliwa kuwa Spika mpya wa Bunge la Tanzania 2015 - 2020

Picha: Habarileo.co.tz

Hongera Mh Job Ndugai kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Spika mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha 2015 - 2020. Ushindi huo unathibitisha imani kubwa walionayo wabunge katika kusimamia chombo hiki muhimu kwa ustawi wa nchi yetu. Ni imani ya blogu hii utatimiza majukumu yako ikiwemo kuishauri na kuisimamia serikali ili Tanzania ipige hatua kubwa ya maendeleo. Hongera sana Mh Ndugai, Mwenyezi MUNGU akuongoze ili uliongoze Bunge hili kwa hekima, amani na upendo kwa kuzingatia kanuni, sheria na katiba.

No comments:

Post a Comment