Hongera sana Mhe Samwel Sitta kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Mhe. Sitta ameshinda kwa kupata kura nyingi dhidi ya mpinzani wake Mhe Hashim Rungwe katika uchaguzi huo. Ushindi wa Mhe Sitta ni mkubwa kwa maana amepata zaidi ya asilimia 80% ya kura zote zilizopigwa na wajumbe wa Bunge la Katiba.
Hakika blogu hii inampongeza sana Mhe Sitta kwa ushindi huo mkubwa. Wajumbe wa Bunge la Katiba bila kujali itikadi za kisiasa na siasa za makundi wamekuwa na imani na Mhe Sitta. Aidha blogu hii inawapongeza wajumbe wote kwa kumchagua Mhe Sitta kuwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Blogu hii inaamini chini ya Mhe Sitta, Bunge hili litaendeshwa vizuri na kufanikiwa kupitisha rasimu ya katiba ambayo itapelekwa kwa wanachi kupigiwa kura.
Mchakato huu wa upatikanaji katiba mpya ni muhimu sana kwa taifa letu. Hivyo kupatikana kwa Mhe Sitta kunatoa imani kwa wananchi wa nchi hii kuwa mchakato katika hatua hii utaenda vizuri.
Picha: Sundayshomari.com
No comments:
Post a Comment