Monday, March 3, 2014

Hongera Young Africans Sports Club aka YANGA kwa kuifunga timu mashuhuri kutoka nchini Misri National Al Ahly jumamosi 01/03/2014 ndani ya uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam

Hongera Dar es Salaam Young Africans aka Yanga kwa kuifunga timu mashuhuri kutoka nchini Misri National Al Ahly. Timu hii ni bingwa wa Afrika kwa sasa. Hakika blogu hii imefurahishwa na jinsi vijana wa jangwani walivyocheza siku ile ya jumamosi 01/03/2014 katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Pia blogu hii inawapongeza viongozi wa Yanga kwa uongozi madhubuti uliopelekea timu kupata ushindi nyumbani. Pia blogu hii inawapongeza makocha wote wa Yanga kwa mbinu za hali ya juu zilizoiwezesha Yanga kupata ushindi huo.

Blogu hii pia inawapongeza mashabiki wa mpira nchini na hasa wale waliojitokeza kuishangilia Yanga. Hakika blogu hii ilifarijika kwa kuona jinsi wapenzi walivyokuwa nyuma ya wachezaji na timu nzima ya Yanga. Blogu hii inaomba viongozi, benchi la ufundi na wachezaji kujiandaa kikamilifu kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika tarehe 09/03/2014 nchini Misri katika jiji la Cairo. Ni vyema wachezaji wakaandaliwa kisaikolojia na kimbinu ili Yanga iweze kusonga mbele. Ikiwezekana mikakati ya ushindi inapidi iandaliwe kama vile kuhakikisha timu inakwenda na maji na chakula chake ama mpishi wake maalum. Pia kuwepo na tahadhari wakati wote ndani ya ardhi ya Misri. Ulinzi uwe asilimia 100%. Pia wachezaji wahakikishe wanakuwa na nidhamu ya hali ya juu na hasa wanapokuwa kwenye eneo lao. Pia watambue kuwa kutakuwa na filimbi zisizo rasmi ambazo zinaweza kuwachanganya wanapokuwa wanaenda lango la timu pinzani. Hapo wanatakiwa kusikiliza filimbi ya refarii tu na si vinginevyo.

Hakika blogu hii imegundua kumbe timu zetu zikiwa na juhudi, nia na malengo pamoja na nidhamu ya kimchezo uwezekano wa kuzifunga timu ziitwazo kubwa barani Afrika upo. MUNGU ibariki Yanga....MUNGU ibariki Tanzania. Mapambano bado yanaendelea!

No comments:

Post a Comment