Vita dhidi ya ujangili nchini Tanzania inastahili kuungwa mkono na wananchi wote wa Tanzania. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete akizungumza na shirika la habari la kimataifa la BBC juu ya juhudi za serikali kupambana na ujangili. Rais ameonyesha dhamira ya kweli ya kupambana na majangili hao. Kumekuwepo na operationi mbalimbali ambazo serikali imefanya kama vile operationi kipepeo na hii ya hivi karibuni ya operationi tokomeza ujangili.
Hakika blogu hii inaungana na serikali pamoja na Mkuu wa nchi katika mapambano dhidi ya vita ya ujangili. Blogu hii inampongeza Mh Rais kwa serikali yake kwa kuutambua mtandao mpana wa ujangili na kuzidi kupambana nao. Hakika ujangili unarudisha nyuma maendeleo ya nchi.
Blogu hii inaviomba vyombo vya ulinzi na usalama kuzidisha kasi ya kuhakikisha majangili wanashindwa ili kuokowa tembo na faru ambao wako hatarini kutoweka. Juhudi kama tokomeza ujangili ilikuwa na lengo zuri sana ingawa kwa namna moja ama nyingine ilileta athari kwa wengine. Blogu hii inaiomba serikali kwa kutumia vyombo vyake kuifufua operationi tokomeza ujangili kwa namna ya kupambana na majangili hawa bila ya kuleta athari kwa wengine.
Nchi yetu inasifika sana kwa utalii. Utalii huu kwa namna moja unategemea uwepo wa wanyama hawa. Utalii huu, unaongeza pato la taifa ambalo linaiwezesha serikali kusukuma maendeleo kwa wananchi. Majangili kuendelea kuuwa tembo na faru ni kuhujumu uchumi wa taifa letu na kuikosesha serikali mapato ya kuwaletea wananchi maendeleo. Tuukatae ujangili kwa kauli moja!
Hebu sikiliza mahojiano ya Mh Rais JK na BBC juu ya juhudi za serikali kutokomeza ujangili.
Picha: Ayoubmzee.blogspot.com
Picha: Journo Tourism
No comments:
Post a Comment