Monday, February 3, 2014

Hongera MBWANA SAMATTA aka SAMA GOAL kwa kuwa mchezaji bora wa klabu ya TP Mazembe 2013

Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta aka "Sama goal" amekuwa mchezaji bora wa klabu ya TP Mazembe kwa mwaka 2013. Klabu ya Tout Puissant Mazembe ni mojawapo ya klabu maarufu barani afrika na yenye mafanikio makubwa.
Aidha, mshambuliaji huyo wa kimataifa toka nchini Tanzania amewashinda wachezaji wenzake maarufu wa klabu hiyo kama vile Solomon Asante pamoja na Robert Kidiaba. Kwa mujibu wa taarifa Samatta alipata kura zipatazo 248. Wengine waliopata kura ni Asante Solomon aliyepata kura 219 akifuatiwa na Robert Kidiaba aliyepata kura 200, Nathan Sinkala aliyepata kura 97 na Rainford Kalaba aliyepata kura 67.
Samatta amekuwa tegemeo la ufungaji wa mabao kwa klabu yake ya TP Mazembe kuanzia Ligi Kuu ya CONGO DRC, Ligi ya Mabingwa Afrika nk.
Blogu hii inampongeza sana SAMATTA na kumuomba aongeze juhudi ili aje siku moja kuwa mchezaji mkubwa kwa ligi kubwa duniani hasa nchini uingereza, hispania, ufaransa nk. Pia blogu hii inawaomba wachezaji wengine wa tanzania wafuate nyayo za SAMATTA ili nao waweze kuitangaza nchi yetu na kuipa mafanikio. 
Blogu hii pia inaiomba TFF kuweka utaratibu mzuri wa soka la vijana kuanzia ngazi ya chini mpaka taifa. Kwa njia hiyo nchi yetu itawapata wakina SAMATTA wengi zaidi na kuiwezesha nchi yetu kuwa tishio barani Afrika. Serikali nayo ina mchango mkubwa kwa kuhakikisha tunakuwa na miundo mbinu ya kisasa kama viwanja vikubwa na vya mazoezi mikoani na wilayani pamoja na kuhakikisha tunaifanya michezo kama somo la lazima katika shule za awali, msingi na sekondari. Maana ya kufanya hivyo ni kuwa sehemu kama shuleni ndipo penye chimbuko la wachezaji wanaojitambua. Pia serikali kupita wizara zake kama elimu na michezo ama utamaduni wanawajibika kuweka sera madhubuti za michezo na kuhakikisha wadau wengine kama mashule, vyama vya michezo, academy nk wanatekeleza sera za serikali kikamilifu.
Picha:in2eastafrica.net

No comments:

Post a Comment