Sunday, February 2, 2014

Hongera Clouds FM radio kwa kurusha matangazo kupitia mtandao wa internet- Radio ya watu

Hongera Clouds FM radio kwa kurusha matangazo kupitia mtandao wa internet. Hakika blogu hii imefurahishwa na juhudi zenu za kuwapasha habari watanzania walioko ndani na nje ya Tanzania. Nikiwa kama mdau wa blogu hii ya tuijenge tanzania nimefurahi sana kupata habari za Tanzania kupitia radio hii kwa njia ya mtandao wa internet nikiwa ulaya nchini Sweden. Nikiwa Sweden nimeweza kusikiliza takribani vipindi vingi vya radio hii hasa kipindi maarufu nikipendacho cha michezo cha saa tatu usiku kiitwacho sports xtra. Mbali na kusikiliza matangazo ya radio hii kupitia internet pia waweza kupata matangazo live vile vile. Hakika watanzania walioko nje ya Tanzania wanajifunia kuwa na radio hii ya kisasa inayokata anga. Na ndio maana ilikuwa ikiitwa mawingu studio enzi hizooo.

Mtanzania yoyote aliye nje ya Tanzania anaweza kupata matangazo ya radio hii kupitia link hii (ustream) ama kupitia kwenye mtandao wa radio hii. Aidha kwa kupitia mtandao wa internet waweza kupata matangazo ya Clouds Tv!! Hakika ukiwa popote pale duniani unapata uhondo na habari toka Tanzania.

Blogu hii inaomba radio nyingine za Tanzania ziingie katika mfumo huu wa kimataifa ili kuwapasha watanzania habari mbalimbali.


Picha: perfecttz.com

No comments:

Post a Comment