Tukitaka maendeleo ya kweli kwa taifa letu ni kulipa kodi. Hivi karibuni serikali kupitia mamlaka ya kodi nchini (TRA) ilianzisha utaratibu wa wafanyabiashara kulipa kodi kupitia mashine za EFD. Ikumbukwe matumizi ya mashine hizi kwa wafanyabiashara umepitishwa na bunge la Tanzania mwaka 2011. Viongozi wengi wamesisitiza matumizi na faida ya mashine hizi za EFD.
Bila kumung'unya maneno, baadhi yetu nchini tumekuwa na utamaduni wa kutopenda kulipa kodi. Kodi ni maendeleo, kodi ndizo zinazojenga miundombinu kama barabara, reli; kodi ndizo zinazowezesha serikali kujenga mashule na kuajiri waalimu wenye sifa; kodi ndizo zinawezesha serikali kujenga hospitali na vituo vya afya pamoja na kuajiri wauguzi na madaktari. Hakika bila kukusanya kodi taifa lolote ikiwemo Tanzania halitapiga hatua.
Baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wagumu kukubali matumizi ya mashine hizi. Kuna baadhi wana sababu za msingi ambazo mamlaka ya mapato TRA inapaswa kuzifanyia kazi. Ila kuna dalili ya baadhi ya wafanyabiashara kwa makusudi wamekuwa hawataki matumizi ya mashine hizi. Hali hii itaifanya serikali kukosa mapato toshelezi ya kuwahudumia wananchi.
Blogu hii inawaomba wafanyabiashara kukubali kutumia mashine hizi kwa ustawi na maendeleo ya taifa letu. Nchi zilizoendelea kama vile Sweden zimefanikiwa kuwaletea wananchi wao maendeleo ya kweli kupitia kodi. Nchi hizo zinakusanya kodi. Moja ya njia nzuri ya kukusanya kodi kwa nchi hizi zilizoendelea ni kutumia mfumo wa mtandao wa kompyuta. Mfumo huu unawezesha kila mlipa kodi (mfanyabiashara/biashara) kulipa kodi. Hapa Tanzania, serikali inajaribu kwenda huko kwa wenzetu, yaani kukusanya kodi kwa njia ya kisasa, yaani kutumia mfumo wa mtandao wa kompyuta. Matumizi ya mashine ya EFD ni mojawapo ya mifumo ya mitandao ya kompyuta ambayo itaiwezesha TRA kukusanya kodi kikamilifu ili kuifanya serikali kupata fedha za kuwaletea wananchi maendeleo.
Blogu hii inaiomba TRA kuzidi kutoa elimu ya umuhimu wa kutumia mashine hizi za kieletroniki za EFD kwa wafanyabiashara. Pia blogu hii inaomba TRA kurekebisha kasoro za msingi zinazotolewa na wafanyabiashara.
Blogu hii inaiomba TRA kuzidi kutoa elimu ya umuhimu wa kutumia mashine hizi za kieletroniki za EFD kwa wafanyabiashara. Pia blogu hii inaomba TRA kurekebisha kasoro za msingi zinazotolewa na wafanyabiashara.

Picha: Barabara kama hizi hujangwa kutokana na kodi (hii picha toka nchini Mauritus inaonyesha jinsi gani nchi ikikusanya kodi vizuri na hasa kwa kutumia mashine za EFD za TRA inavyoweza kupata maendeleo)
No comments:
Post a Comment