Saturday, February 1, 2014

Wawekezaji wa sekta ya madini nchini kulipa kodi ya asilimia 30 kwa mujibu wa sheria

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospiter Muhongo, amesema kuwa wawekezaji wa madini nchini watalazimika kulipa kodi ya asilimia 30 kwa mujibu wa sheria. Awali, wawekezaji walikuwa hawalipi kodi kwa kiasi hicho kwa madai kuwa walikuwa wakipata hasara. Kwa sasa wawekezaji wa sekta ya madini watalazimika kulipa kodi hiyo na kuleta mchango mkubwa kwa taifa.

Profesa Muhongo alisema kwa sasa sekta ya madini kwa sasa inachangia asilimia 3.5 ya pato lote la Taifa. Aidha Profesa Muhongo amesema malengo ya serikali ni kuhakikisha kuwa sekta hii ya madini inachangia zaidi ya asilimia 10 ifikapo mwaka 2025.
Vilevile, lengo la serikali ni kuhakikisha sekta ya madini inaleta mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa. Blogu hii inampongeza Waziri wa Nishati na Madini kwa kauli hiyo ambayo inaleta matumaini kwa taifa letu changa. Ni imani ya blogu hii kuwa sekta ya madini itachochea maendeleo kwa taifa kama sheria hii ya kodi itasimamiwa vyema na serikali na wadau wengine. 

Picha: mwananchi.co.tz

No comments:

Post a Comment