Hakika elimu kwa vitendo ni suala ambalo sisi watanzania na hasa wizara yetu ya elimu inapaswa kulitilia mkazo kwa kiwango kikubwa. Nchini Sweden, wanafunzi wa chekechea na shule za msingi wanajifunza kwa vitendo kwa kiasi kikubwa. Tanzania, tulikuwa tunaita elimu ya kujitegemea. Nakumbuka zamani miaka ya semanini hapa Tanzania kulikuwa na masomo ya sayansi kimu, maarifa ya nyumbani n.k. Nchini Sweden licha ya maendeleo makubwa waliyonayo bado hawajaacha kuwafundisha watoto wao maarifa ya nyumbani kama vile kushona, kuranda, kuchonga, kuchora n.k.
Blogu hii inaiomba serikali ya Tanzania kupitia wizara husika kurudisha elimu kwa vitendo katika masomo tunayofundisha wanafunzi wetu. Kuna visingizio kwa baadhi ya wadau wa elimu kuwa hatuna vitendea kazi! Si kweli kwani kama mdau wa blogu hii nimeshuhudia kwa macho yango baadhi ya vifaa wanavyotumia sisi hapa Tanzania tunaweza kuvipata bila gharama yoyote. Vitu kama miti, udongo, maji, moto, uzi, kamba, majani, chupa zilizotumika n.k ni vitu ambavyo vinaweza kutumika kuwasaidia wanafunzi kuelewa somo vizuri.
Chupa mbili tupu zinatumika katika somo la fikizia, vitambaa vilivyotumika na uzi vinaweza kutumika kutengeneza midoli kwa wanafunzi.
Blogu hii inaomba watanzania hasa wadau wa elimu wabadilike na tuwafundishe wanafunzi kwa vitendo. Bila elimu ya vitendo itakuwa vigumu kwa wanafunzi wetu kuelewa mada ngumu. Elimu ya kujitegemea itiliwe mkazo sana na wakaguzi wa shule wafuatilie kuhakikisha wanafunzi wanafundishwa kwa vitendo ili kudumisha dhana ya elimu ya kujitegemea.

Picha: Moja ya shule ya msingi nchini Sweden, ambapo wanafunzi wanajifunza mpaka useremala!

Picha: Moja ya shule ya msingi nchini Sweden, ambapo wanafunzi wanatumia kamba,
mabaki ya miti (fimbo na vipande vya mbao) kaika kujifunzauseremala!

Picha: Moja ya shule ya msingi nchini Sweden, ambapo vipande vya nguo vinatumika kutengeneza
midoli na vitu vingine vya ushonaji!
No comments:
Post a Comment