Sunday, February 2, 2014

Hongera serikali ya Tanzania kwa kutoa punguzo la kuunganisha umeme vijijini hadi kufikia TShs 27,000 tu!

Serikali ya Tanzania imepunguza gharama za kuunganisha umeme kwa maeneo ya vijijini. Kabla ya punguzo hilo gharama ilikuwa TShs 177,000 tu lakini sasa ni TShs 27,000 tu. Aidha punguzo la awali lilikuwa kwa mikoa ya Lindi na Mtwara lakini kwa sasa punguzo hilo ni kwa nchi nzima. Hakika blogu hii imefurahishwa na juhudi hizi za serikali za kusambaza umeme vijijini kupitia REA. Maendeleo ya kweli yanatoka vijijini ambako ndiko kuna uzalishaji kupitia kilimo na mifugo.

Pia blogu hii inaamini wananchi waishio vijijini watatumia fursa hii ili kuwa na umeme kwa ajili ya matumizi ya kawaida na kimaendeleo. Kupitia juhudi hizi za serikali ni rahisi kwa wawekezaji kuamia vijijini kutokana na fursa ya umeme. Hii itachochea maendeleo kwa kuwa ni rahisi kuwa na viwanda vidogo na vikubwa vya usindikaji mazao. Hii itaongeza thamani ya mazao toka kwa wakulima ambao wengi wao wanaishi vijijini.


Picha:simbadeo

No comments:

Post a Comment