Monday, February 10, 2014

Uwepo wa maktaba mashuleni unaongeza maarifa na ujuzi kwa walimu na wanafunzi.

Maktaba katika mashule ni suala ambalo Tanzania inatakiwa kulitilia mkazo. Nchini Sweden, takriban shule zote kuanzia chekechea, msingi mpaka sekondari kuna maktaba za shule. Maktaba hizi zinawasaidia wanafunzi kupata vitabu, majalida na machapisho mbalimbali kwa ajili ya masomo yao. Vile vile walimu nao hupata wasaa wa kutumia maktaba kwa ajili ya kuandaa mada mbali mbali za masomo kwa ajili ya wanafunzi.

Tanzania tunatakiwa kuiga mfano huo wa kuwa na maktaba za kisasa zenye vitabu, machapisho na majalida kwa ajili ya wanafunzi na walimu. Hii itawasaidia sana wanafunzi kuongeza ujuzi na maarifa wa mambo wanayojifunza shuleni.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inabidi itilie mkazo suala la maktaba mashuleni kwa kuweka vitabu, majalida na machapisho kulingana na mitaala husika na pia kuhakikisha wanaajili wakutubi waliohitimu toka taasisi zinazotoa mafunzo ya kimaktaba. Hii itasaidia kuwezesha wanafunzi na walimu kupata msaada wa kitaalamu toka kwa wataalamu (wakutubi).

Pia ni vyema kwa serikali kuwa na sera ya kuwa na maktaba katika shule zetu na kuhakikisha wakaguzi wa shule wanakagua uwepo wa maktaba za shule kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu.


Uwepo wa maktaba mashuleni unaongeza maarifa na ujuzi kwa walimu na wanafunzi.


Picha: Mojawapo ya MAKTABA katika shule ya msingi nchini Sweden

No comments:

Post a Comment