Tuesday, March 25, 2014

Hongera Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kutangaza mauzo ya nyumba 214 Mwongozo, Kigamboni jijini Dar es Salaam

Hongera Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kutangaza mauzo ya nyumba 214 Mwongozo, Kigamboni jijini Dar es Salaam. Kwa mara nyingine tena leo Jumanne, Machi 25, 2014 Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limewatangazia wananchi mauzo ya nyumba 214 zinazojengwa eneo la Mwongozo, Kigamboni Jijini Dar es salaam. Maelezo hayo yalitolewa na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara, Bw. David Shambwe kwenye kikao na waandishi mbalimbali wa habari nchini. 

Hakika blogu hii imefurahishwa na juhudi za shirika hili la umma la kuwapatia wananchi wa Tanzania maisha bora kupitia ujenzi wa nyumba bora. Blogu hii inapenda kuliomba shirika hili liongeze kasi ya ujengaji, uuzaji na ukodishaji nyumba kwa ajili ya watanzania.Hakika blogu hii inapendezwa na uongozi imara wa Shirika hili la umma.

Pia blogu hii inaomba shirika la nyumba liende kwenye taasisi za binafsi na serikali na kuingia mikataba ya muda mrefu na wafanyakazi kupitia waajiri wao ili wananchi wengi waweze kupata nyumba bora za kuishi. Mfano, kuna wafanyakazi wa serikali ambao wana umri wa miaka 25 na ambao wanaweza kuingia mkataba na shirika la nyumba kwa miaka hata 35 kwa kukatwa asilimia fulani kwenye mshahara wakati huo huo mhusika akiwa kwenye nyumba yake tayari. Hii ni faida kubwa kwa mfanyakazi wa umma ama wa binafsi maana hata kama atakuwa hajamaliza mkopo bado atakuwa anaishi kwenye nyumba hiyo kana kwamba analipa kodi kwa kiasi kidogo. 

Kwa habari zaidi kuhusu taarifa hii na kwa mtanzania anayetaka nyumba hizi, Tembelea link hii ya Shirka la Nyumba la Taifa (NHC) kwa maelezo zaidi.


Picha: http://www.nhctz.com/mwongozo/

No comments:

Post a Comment