Thursday, April 27, 2017

Hongera Mh Ummy Mwalimu kwa kumwakilisha vyema Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwenye kongamano la kimataifa la jinsia

Hongera Mh Ummy Mwalimu kwa kumwakilisha Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwenye kongamano la kimataifa la jinsia" DUCE 1st International Conference on Gender in Higher Learning Institutions". Madhumuni ya kongamano hili la kimataifa ni kuibua mambo mbalimbali yahusuyo jinsia kwa mtizamo wa taasisi za elimu ya juu katika kutetea usawa wa kijinsia na haki za kibinadamu. 
Image may contain: 1 person, standing, car and outdoor
Blogu hii inatoa pongezi kwako hasa kwa hotuba nzuri sana. Hakika blogu hii imefuatilia hotuba uliyoitoa na kuzifanya taasisi za elimu ya juu (vyuo vikuu ikiwemo DUCE) kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo " ongezeko la wanafunzi wa kike na kiume kupitia elimu bure itolewayo na serikali mpaka kidato cha nne". Pia blogu hii imefurahishwa na kauli ya kuwahimiza wasichana na wanawake kuwa ELIMU ndio kila kitu sio sura au umbo zuri. 
Image may contain: 6 people, people standing and outdoor

Image may contain: 6 people, people standing, suit, wedding and outdoor
Aidha umesisitiza umuhimu na ulazima wa kutokatisha masomo watoto wa kike wanaopata mimba mashuleni. Hakika hili ni jambo jema na litaokoa wasichana wengi ambao wangekosa masomo kwa ajili ya mimba. 


Image may contain: 2 people, people standing

Image may contain: one or more people
Tatizo la mimba za watoto wa kike linaenda hasa kwa familia maskini nchini. Kitendo cha kutetea ELIMU kwa mtoto wa kike ni suala linalopaswa kuungwa mkono na kila mwananchi nchini Tanzania wakiwemo wabunge, madiwani, watunga sera, wataalamu wa elimu nk.
Image may contain: 3 people, people sitting

Image may contain: 6 people, crowd

Hongera sana Mh Ummy kwa kumwakilisha vyema Mama Samia Suluhu Hassan.


Image may contain: 3 people, people standing

No comments:

Post a Comment