Sunday, April 16, 2017

Hongera serikali ya Tanzania chini ya Rais Dkt Magufuli kwa uzinduzi ujenzi wa maghorofa ya Magomeni jijini Dar es Salaam

Tokeo la picha la magufuli MAGOMENI
Picha: ccm/ikulu
Hongera serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa uzinduzi ujenzi wa maghorofa ya Magomeni jijini Dar es Salaam. Siku ya jumamosi ya tarehe 15 Aprili 2017 Mh Rais aliweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa maghorofa mbalimbali kwa ajili ya wakazi wa Magomeni KOTA. Hakika manthari ya jiji la Dar es Salaam itabadilika mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huu mkubwa ambapo licha ya kuwahifadhi wakazi 644 waliokuwa wa Magomeni KOTA pia watu wengine watapata fursa ya kuishi katika majengo hayo. 


Blogu hii inampongeza Rais na inamwomba azidi kuwaletea watanzania maendeleo kupitia ujenzi wa makazi bora kwa gharama nafuu. Katika nchi zilizoendelea ujenzi wa namna hii ndio umeboresha makazi ya watu na kwa Tanzania ya Magufuli INAWEZEKANA.


No comments:

Post a Comment