Monday, August 5, 2013

Hongera Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutokomeza malaria toka asilimia 25 mpaka chini ya 1

Hongera serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kupambana na kutokomeza malaria. Hakika juhudi hizi ni za kupongezwa maana ZANZIBAR imeweza kupambana na malaria kutoka kiwango cha asilimia 25 mpaka kufikia asilimia chini ya 1. Hata rais mstaafu wa Marekali Bill Clinton ameona na kutambua juhudi hizo na kuahidi kuzidi kuisaidia ZANZIBAR. Ugonjwa wa malaria ndio chanzo kikuu cha vifo kusini mwa jangwa la sahara na wanaoathilika zaidi ni watoto walio chini ya miaka mitano. Juhudi hizi zifanywe pia na upande wa pili wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ili kuokoa vifo vinavyoweza kuzuilika.

Picha: sundayshomari.com

No comments:

Post a Comment