Thursday, August 1, 2013

Hongera TCRA kwa kuzindua kampeni ya kuelimisha wananchi juu ya matumizi mazuri ya mawasiliano

Hongera TCRA kwa kuzindua kampeni nzuri ya kuelimisha jamii ya kitanzania juu ya matumizi mazuri ya mawasiliano. Katika uzinduzi huo TCRA imewatahadharisha wananchi kwa ujumla kutotumia fursa ya kukua kwa kasi kwa teknolojia ya mawasiliano vibaya, kama ilivyoanishwa katika Sheria ya Kielectroniki na Posta ya mwaka 2010. Blogu hii inapenda kuipongeza TCRA na mkurugenzi wake mkuu kwa kampeni hii. Pia blogu hii inapenda kampeni hii iwe endelevu.
Picha na chanzo cha habari: ippmedia.com 


No comments:

Post a Comment