Tuesday, July 30, 2013

Uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kyaka - Bugene mkoani Kagera uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete

Uzinduzi wa ujenzi wa barabara za mikoani hasa mikoa ya pembezoni ni jambo linalochochea maendeleo ya taifa. Blogu hii inatoa pongezi kwa uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kyaka mpaka Bugene uliofanyika Bunazi mkoani Kagera na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete. Mbali na kuipongeza serikali kwa juhudi hizi pia blogu hii inapenda kuomba barabara zingine zizidi kujengwa.

Aidha blogu hii inaiomba serikali kuwa na mikakati endelevu ya kuzuia uharibifu wa barabara zinazojengwa kwa gharama kubwa. Kuwepo na faini kubwa na kali kwa wale wote wanaokiuka sheria katika utunzaji na utumiaji bora wa barabara hasa za kiwango cha lami na changarawe.

Picha hii ni kutoka DailyNews Online Edition.











No comments:

Post a Comment