Monday, July 15, 2013

BUSARA toka kwa Mkubwa Kambi - TAIFA Stars isikate tamaa! CHAN twaweza kwenda!!

Mwanzo wa nukuu toka kwa Mkubwa Kambi
"Kwa wale wapenzi wa soka someni kwa makini mkasa huu,1983 Waganda hawa hawa walitufanya mbaya pale National Stadium walitupiga kidude katika pambano la kwanza, washabiki walishikwa na hasira kweli wachezaji iliwalazimu kutoka uwanjani saa tatu usiku, kwenye kichwa cha habari cha gazeti la mfanyakazi James Nhende aliandi, "Mogela afunikwa" pamoja na kebehi kibao kutoka kwa mashabiki, Zamoyoni Mogella alimpiga mwandishi yule na file likafunguliwa polisi.
Baada ya siku mbili tatu Charles Bonface "Mkwasa", Zamoyoni Mogella, Lilla Shomari wakatangaza kujiuzulu kuchezea Stars, FAT (TFF) nayo na serikali waliona hakuna haja tena timu ya Taifa kwenda kucheza mechi ya marudiano kule Uganda kwani ilikuwa ni gharama (ikumbukwe enzi zile hakuna udhamini).
Baadhi ya wadau wa soka walijaribu kuzungumza na wachezaji tatizo lilikuwa nini, nao waliitaja moja ya sababu ni upangaji wa timu, wakati huo ilikuwa chini ya Kocha Geff Hudson (muingereza).
Wachezaji wakaketishwa chini pamoja na kocha wao wakafikia muafaka, serikali ikaombwa igharamie usafiri vijana waende Uganda na wale wachezaji waliotishia kujiuzulu walirudi kundini. Vijana wale wakapatiwa ATC wakaenda zao Uganda na kikosi cha timu walikipanga wenyewe kocha akiwa msimamizi tu, ndani ya dakika 15 Uganda ameshapigwa goli mbili za Zamoyoni Mogella, Celestine "Sikinde" Mbunga akashindilia msumari wa mwisho, hadi mwisho Sisi 3 wao 1 tukasonga mbele.

Kwenye soka hakuna lisilowezekana, tatizo la wachezaji wetu wa kizazi hiki wamekosa kujiamini hivyo kushindwa kuongea hata kama tatizo wanaliona, nafasi naamini bado tunayo tujipange tuache mipango ya zima moto wiki mbili zinatosha kumuua mganda.

Kila la heri Taifa Stars, jitambueni."
Mwisho wa nukuu toka kwa  Mkubwa Kambi

No comments:

Post a Comment