Tuesday, July 23, 2013

HONGERA Mh. Jerry Silaa kwa ujenzi wa kivuko cha miguu kwenda ulongoni

Kwa mujibu wa Jerry Silaa ambaye ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Kata ya Gongo la Mboto amesema ujenzi wa kivuko cha miguu kwenda ulongoni kuanza punde kwa ufadhili wa diwani wa kata ya Gmboto. Hakika msomaji unaweza kuona kama jambo hili ni dogo lakini lina manufaa makubwa kwa jamii yetu. Kama madiwani wote nchini wakifanya juhudi kama hii kwa hakika nchi yetu itapiga hatua kubwa ya maendeleo. Blogu hii inatambua mchango wako na pia inakuomba uzidi kuiletea maendeleo kata yako na manispaa kwa ujumla.

Kwa kuwa shabaha ya blogu hii ni pamoja na mambo mengine kupongeza juhudi za maendeleo zinazofanywa na watanzania kwa ajili ya watanzania na kwa kutambua mchango wako blogu hii ingependa wananchi wajue huyu Mh Jerry ni nani? Fungua hapa


 
  Chanzo: Mh. Jerry Silaa

No comments:

Post a Comment