Pongezi za dhati kwa Dr Stergomena Tax kwa kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa SADC kwa kipindi cha 2013 - 2017
Mwanzo wa kunukuu "Ni
furaha kubwa kwangu kwa Dr. Stergomena Tax (Mwanamke toka Tanzania)
kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa SADC kwa kipindi cha 2013 -2017. Hii ni
mojawapo ya vielelezo vingi kuwa WANAWAKE WANAWEZA! Hongera sana Dr.
Tax, Hongera sana Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe Benard Membe kwa kazi
nzuri. Hongera nyingi zaidi kwa Mhe. Rais, Jakaya Kikwete kwa kuwekeza
na kuamini kwa dhati katika Uongozi wa Wanawake (Women Leadership). Sifa
nzuri ya Tanzania inazidi kupaa! Kila la kheri Dr. Tax ktk Utekelezaji
wa Majukumu yako Mapya." Mwisho wa kunukuu (Mh Ummy Mwalimu - Mbunge, Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto)
Blogu hii inapenda kutoa pongezi za dhati kwa Dr Stergomena Tax kwa kuaminiwa na kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa SADC. Pia blogu hii inapenda kuwashukuru waliochangia mafanikio ya mama huyu hasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete. Pia blogu hii inapenda kumshukuru Mh Ummy Mwalimu kwa taarifa hii njema kwa watanzania. HAKIKA WANAWAKE WANAWEZA, TUZIDI KUWAAMINI!
Picha:http://www.wavuti.com
No comments:
Post a Comment