Hongera Timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 kwa ushindi mnono mlioupata leo kwenye uwanja wa taifa.
Mchezo wa leo ni harakati za Timu yetu kuwania kuingia fainali za wanawake zitakazofanyika nchini Canada mwakani kupitia kanda ya Afrika. Timu yetu imepata ushindi wa mabao 10 kwa 0!
Hakika Timu hii imetutoa kimasomaso licha ya wadau wa michezo nchini kuwa bize na uchaguzi wa bodi ya ligi na ule uchaguzi wa shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF).
Lakini blogu hii inaungana na wadau wa michezo nchini hususan kandanda kuipongeza Timu yetu ya wanawake kwa ushindi mkubwa walioupata.
Tunaomba wale wote walio bize na uchaguzi wahakikishe wakishachaguliwa wanatilia mkazo uanzishwaji wa ligi ya wanawake nchini Tanzania ili tuweze kupata wachezaji bora watakaoliwakilisha taifa katika mashindano ya kimataifa.
Heko kwa kututoa kimasomaso
ReplyDelete