Hongera sana klabu ya YANGA kwa kuwa na wazo la uwanja wa kisasa ambao michoro ya awali ishachorwa na wataalamu. Pili blogu hii ina upongeza uongozi wa klabu ya YANGA kwa kuonana na Mshahiki Meya wa Manispaa ya Ilala na kutuma maombi ya kuongeza eneo la kiwanja. Hakika juhudi hizi zinastahili kuungwa mkono na wadau wote wa michezo hususan mpira wa miguu aka kandanda AMA kabumbu. Kwa mujibu wa mtandao wa YANGA Meya wa Manisapaa ya Ilala jijini Dar es salaam mstahiki Jerry Slaa leo amepokea maombi ya klabu ya Young Africans kuhusu kuomba eneo la ziada kwa ajili ya kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa uwanja wa kisasa eneo la jangwani.
Juhudi hizi sio ndogo na zinapaswa kuendelezwa. Wapo watu wanafikiri hii ni ndoto la hasha bali inawezekana kwa Klabu kama YANGA kujenga uwanja wa kisasa. YANGA ina wadau wengi sana ndani na nje ya nchi.
Kinachohitajika ni kwa YANGA kuunda kamati ya ujenzi itakayowashirikisha wadau wa YANGA wakiwemo wataalamu mbalimbali wa ujenzi, wataalamu wa masoko, wataalamu wa ardhi na miundombinu, makocha, wachezaji wa zamani, wafanyabiashara, wanasiasa bila kusahau wakeleketwa YANGA wakiwemo na wanachama na baadhi ya wajumbe toka kwenye uongozi wa YANGA. Muhimu kamati iwe na watu makini na wanaoaminika ili moja ya jukumu ni kuandaa mpango mkakati na pia kuusimamia mpango huo. Mpango huo uonyeshe roadmap ya kupata fedha na na namna pesa itakavyotumika.Klabu nyingine zinapaswa kuiga mtizamo wa YANGA ili Tanzania ipige hatua kwenye maendeleo ya soka.
Kwa habari zaidi bofya hapa.
No comments:
Post a Comment