Siku ya tarehe 11 oktoba mwaka huu ilikuwa siku ya kimataifa ya
Mtoto wa Kike. Mh. Ummy Mwalimu Naibu waziri wa maendeleo ya wanawake, jinsia
na watoto alitumia siku hiyo jijini Tanga kuzindua Mradi wa kuwajengea
uwezo wasichana wa mkoa wa Tanga chini ya Taasisi ya Tanga Women Development
Initiative (TAWODE).
Mradi huu utakaotekelezwa katika Wilaya za Pangani, Muheza, Mkinga, Lushoto na Tanga Mjini, umelenga kuchochea uwezo na ubora wa wasichana wenye umri wa miaka 10-24 kutambua weledi na umuhimu wao kwa maendeleo yao na ya jamii zao. Kupitia Mradi huu Mh. Ummy na wenzake wamedhamiria kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wasichana waliopo katika shule za Serikali za Msingi na Sekondari, kuboresha hali ya afya ya uzazi, kupunguza mimba za mapema, ndoa za utotoni na maambukizi ya virusi vya ukimwi. Aidha wamepanga kuwafikia moja kwa moja wasichana 16,000 na zaidi ya 100,000 kupitia njia mbalimbali ikiwemo mabango, Radio jingles (Mwambao FM 106.0), matamasha ya wasichana nk. Aidha Wasichana 1,000 waliopo shuleni na wanaoishi katika mazingira magumu wataingizwa katika Mfuko wa Bima ya afya ili kuweza kupata huduma za afya bure. Ni imani ya Mh. Ummy kuwa jitihada hizi zitachochea maendeleo ya wanaTanga kwa jumla.
Blogu
hii inamwomba Mh. Ummy kupitia wizara yake kuweka sheria kali zinazowalinda
watoto mfano sheria zinazokataza watu wenye umri mkubwa kufanya ngono na
vitendo vya kingono na watoto wadogo chini ya miaka 16 ama 18. Sheria hizi zipo
kwa wenzetu na ni kali ambazo zinawalinda watoto hasa wa kike na watu
wajulikanao kama "sugar dad". Hakika zipo sheria nyingi ambazo
kupitia wizara husika wanaweza kuziingiza kwenye system
Mgeni rasmi alikuwa Mhe Chiku Galawa, Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Kupitia mradi huu Mh. Ummy ametekeleza kwa vitendo dhamira yake kama
kiongozi - aliyechaguliwa na wanawake wa mkoa wa Tanga katika kuchangia na
kuboresha maisha ya wanawake wa mkoa wa Tanga.
Mradi huu utakaotekelezwa katika Wilaya za Pangani, Muheza, Mkinga, Lushoto na Tanga Mjini, umelenga kuchochea uwezo na ubora wa wasichana wenye umri wa miaka 10-24 kutambua weledi na umuhimu wao kwa maendeleo yao na ya jamii zao. Kupitia Mradi huu Mh. Ummy na wenzake wamedhamiria kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wasichana waliopo katika shule za Serikali za Msingi na Sekondari, kuboresha hali ya afya ya uzazi, kupunguza mimba za mapema, ndoa za utotoni na maambukizi ya virusi vya ukimwi. Aidha wamepanga kuwafikia moja kwa moja wasichana 16,000 na zaidi ya 100,000 kupitia njia mbalimbali ikiwemo mabango, Radio jingles (Mwambao FM 106.0), matamasha ya wasichana nk. Aidha Wasichana 1,000 waliopo shuleni na wanaoishi katika mazingira magumu wataingizwa katika Mfuko wa Bima ya afya ili kuweza kupata huduma za afya bure. Ni imani ya Mh. Ummy kuwa jitihada hizi zitachochea maendeleo ya wanaTanga kwa jumla.
Hakika blogu hii imefurahishwa sana na Juhudi azifanyazo Mh.
Ummy na wenzake. Blogu hii inamwomba Mh. Ummy azidi kuongeza Juhudi hizi ndani
ya mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla. Blogu hii pia bado inatambua mchango
wa Mh. Ummy nchini Tanzania katika kusimamia masuala ya wanawake na watoto.



No comments:
Post a Comment