Thursday, October 24, 2013

Hongera Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi pamoja na DUCE kwa kujenga kituo maalum "Teachers Professional Center"

 
 


Hongera serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kujenga kituo maalum katika chuo kikuu kishiriki cha DUCE kiitwacho "Teachers Professional Center". Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Gharib Bilal alikuwa mgeni rasmi katika halfa hiyo ya uzinduzi iliyofanyika Jumatano ya tarehe 23 mwezi wa kumi mwaka 2013.

 

Aidha kama mdau nilipata fursa ya kutoa mada mbele ya Makamu wa Rais Mh Gharib Bilal jinsi gani kituo cha "Teacher Professional Center" kinachomilikiwa na DUCE kinavyoweza kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kuchangia ubora wa Elimu nchini na hasa kuweza kuwapa maarifa na ujuzi walimu (in-service teachers) kupitia Teknolojia ya kisasa ili kuongeza maarifa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini na kuongeza ufaulu. 

 

Uzinduzi wa kituo hiki unaenda pamoja na kauli mbiu ya "Big Results Now" yaani "Matokeo Makubwa Sasa" katika sekta ya elimu nchini Tanzania.

 

Blogu hii inapenda kuipongeza serikali ya Tanzania chini ya Mh Rais Jakaya Kikwete kwa ujenzi wa kituo hiki maalum kitakacho chochea kasi ya elimu nchini na hasa kitakachokuwa kikitumika kutoa mafunzo kwa walimu walio makazini kupitia Teknolojia ya kisasa. Aidha blogu hii inakipongeza chuo kikuu kishiriki cha Elimu DUCE kwa kuweza kutekeleza ujenzi wa kituo hiki. Vile vile blogu hii inawapongeza wadau na wafanyakazi wa DUCE pamoja na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika kusimamia ujenzi wa kituo hiki.

 

Pia blogu hii inatoa pongezi na shukrani za pekee kwa Benki ya Dunia (World Bank) kupitia mpango mahsusi uitwao "Science Technology and Higher Education Program (STHEP) " uliofanikisha miradi mingi nchini kwenye sekta ya elimu juu ukiwemo mradi huu wa wa ujenzi wa  "Teacher Professional Center" ndani ya chuo kikuu kishiriki cha DUCE.

 

Blogu hii inaomba kituo hiki kitunzwe na pia kitumike kikamilifu ili kukizi lengo la kituo chenyewe pamoja na kufikia malengo ya BIG RESULTS NOW! Pamoja tutafika!
 

 







 



 


No comments:

Post a Comment