Nchini Australia katika mji wa Melbourne, vijana wengi waliokosa fursa ya kuendelea na masomo ya juu yaani kwenda vyuo vikuu huingia katika mafunzo haya ya ufundi kwa vitendo. Mafunzo haya huku Australia yanaitwa Vocational Education & Training (VET). Mafunzo haya kwetu Tanzania yanaendeshwa na VETA.
Mafunzo haya ni muhimu kwa taifa lolote hasa Tanzania maana yanatoa na kuzalisha nguvukazi yenye ujuzi mbalimbali kuanzia wahudumu wa hoteli, mafundi wa magari na mashine ndogo na kubwa, wajenzi wa barabara na madaraja, wajenzi wa majumba nk.
Mafunzo haya ni muhimu kwa taifa lolote hasa Tanzania maana yanatoa na kuzalisha nguvukazi yenye ujuzi mbalimbali kuanzia wahudumu wa hoteli, mafundi wa magari na mashine ndogo na kubwa, wajenzi wa barabara na madaraja, wajenzi wa majumba nk.
Uchumi wa nchi yoyote hapa duniani unategemea watu wa aina hii. Hata wale vijana wanaomaliza vyuo vikuu bado na wao wanatakiwa kupata mafunzo haya ya ufundi kwa vitendo ili kupata ujuzi wa kazi. Vijana toka vyuo vikuu huwa ni wazuri kwenye eneo la nadharia (theory) lakini huwa na upungufu kwenye eneo la vitendo. Hivyo kwa wenzetu huwa wanawahimiza wanafunzi wa vyuo vikuu kujiunga na vyuo vya ufundi kwa vitendo kupata ujuzi kwa vitendo.
Blogu hii inaomba mafunzo haya yatiliwe mkazo ili taifa letu liwe na wajuzi wa kazi kwa vitendo na kuifanya Tanzania kupiga hatua kubwa ya maendeleo.
Blogu hii pia inaiomba serikali ya Tanzania kutenganisha shughuli za VETA na kuwa taasisi ya kutoa mafunzo (service provider) pekee na kuanzisha taasisi nyingine ya kusimamia (regulator) ili kuwe na ufanisi katika mafunzo kwa vitendo (vocational skills training). Pia kunaweza pia kuwa na taasisi nyingine ya kusaidia hasa katika masuala ya utoaji fedha na vifaa kwa ajili ya mafunzo na usimamizi wa hayo mafunzo.
Kwa maneno mengine kuna kuwa na mfumo wa namna hii
Service Provider - Regulator - Facilitator
Kwa sasa shughuli zote hizi zinafanywa na VETA, hivyo inakuwa vigumu kuendesha kwa ufanisi yaani kutoa mafunzo kama "service/training provider", kusimamia mafunzo "regulator", kusaidia mafunzo kifedha na vifaa "facilitation"
Kitu cha muhimu kukumbuka ni kuwa kuna vyuo vingi vya VETA nchini vinavyoendeshwa na VETA yenyewe na pia kuna vyuo vingine vya binafsi vinavyosimamiwa na VETA.
Blogu hii inaona kuwa kukiwa na mgawanyo wa majukumu, fani ya ufundi kwa vitendo (vocational education training) hapa nchini itapiga hatua kuwa na kuchangia maendeleo ya Taifa.
Kwa maneno mengine kuna kuwa na mfumo wa namna hii
Service Provider - Regulator - Facilitator
Kwa sasa shughuli zote hizi zinafanywa na VETA, hivyo inakuwa vigumu kuendesha kwa ufanisi yaani kutoa mafunzo kama "service/training provider", kusimamia mafunzo "regulator", kusaidia mafunzo kifedha na vifaa "facilitation"
Kitu cha muhimu kukumbuka ni kuwa kuna vyuo vingi vya VETA nchini vinavyoendeshwa na VETA yenyewe na pia kuna vyuo vingine vya binafsi vinavyosimamiwa na VETA.
Blogu hii inaona kuwa kukiwa na mgawanyo wa majukumu, fani ya ufundi kwa vitendo (vocational education training) hapa nchini itapiga hatua kuwa na kuchangia maendeleo ya Taifa.
No comments:
Post a Comment