Sunday, May 14, 2017

Asante Mh Nyarandu, Samaritan's Purse na Serikali kwa kusaidia kuwapeleka watoto walionusurika na ajali Marekani kwa matibabu zaidi

Image may contain: 13 people, crowd, wedding and outdoor
Kwa hili la kusaidia kupeleka watoto watatu Marekani kwa ajili ya matibabu ni jambo la kupongezwa. Mh Lazaro Nyarandu, Mbunge wa Singida Kaskazini, Shirika la Kujitolea la Marekani Samaritan's Purse na Serikali ya Tanzania kwa hili mnastahili pongezi za dhati kabisa. 

No automatic alt text available.
Watoto hawa ni majeruhi wa ajali iliyopoteza uhai wa watoto, walimu na dereva wa shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha. Takribani zaidi ya watu thelathini walipoteza maisha wengi wao wakiwa wanafunzi wa darasa la saba waliokuwa wakielekea Karatu toka Arusha kwa ajili ya mitihani ya ujirani. 

Image may contain: outdoor
Blogu hii pia inawashukuru wafadhili (Samaritan's Purse) wa safari hii ya kwenda nchini marekani kwa matibabu zaidi. Aidha blogu hii inaishukuru Serikali ya Tanzania katika kufanikisha hili na kwa kukubali watoto hawa waende nje kwa matibabu zaidi.

Image may contain: sky, cloud and outdoor

No comments:

Post a Comment