
Picha: Viongozi wakuu wa TAAA waliochaguliwa VETA Mikumi 6 Mei 2017. Kutoka kulia ni
Rais ndugu Makassy, Makamu wa Rais Ms Mary Awinia, Katibu ndugu Bonface Kyaruzi
na Naibu Katibu ndugu Sarah Dotto
Hongera viongozi wapya wa Tanzania Australia Alumni Association (TAAA) kwa kuchaguliwa kuongoza chama hiki juzi 6 Mei 2017 VETA Mikumi, Morogoro. TAAA ni chombo kinachoundwa na wanafunzi waliosoma nchini Australia.

Picha: Wanyama ndani ya Mikumi National Park toka VETA Mikumi 7 Mei 2017
Lengo la TAAA ni kuwaunganisha pamoja wanafunzi waliosoma nchini Australia ili kuiletea Tanzania maendeleo ya kweli kupitia Elimu, Ujuzi na Maarifa toka nchini Australia. Viongozi wa TAAA waliochaguliwa ni Rais ndugu Charles Makassy, Makamu wa Rais ndugu Mary Awinia, Katibu ndugu Boniface Kyaruzi, Naibu Katibu ndugu Sarah Dotto na Mweka Hazina ndugu Nzamba. Aidha TAAA imepata wajumbe watano wa kamati ya utendaji nao ni ndugu Geofrey Felix Kalumuna, Boniphace Paul, Henry Mditi, Pamela Levira na Robert Mashinji.

Picha: Viongozi wakuu wa TAAA pamoja na wajumbe watano wa kamati ya utendaji nje ya Mikumi National Park 7 Mei 2017
Blogu hii inaomba waliochaguliwa kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza malengo ya TAAA na kuiletea Tanzania maendeleo ya kweli. Blogu hii inaamini kuwa viongozi na wanachama wa TAAA wana elimu, ujuzi na maarifa katika kuchochea maendeleo ya Tanzania kwa kasi.

Picha: wakati wa mkutano, VETA Mikumi, Morogoro Mei 6, 2017
No comments:
Post a Comment