
Hongera Mwajuma Kinyemi (Mc Kinyemi) kwa kuhamasisha wanawake katika ujasiriamali siku ya mei mosi.

Hakika blogu hii imefurahishwa sana kwa jinsi ulivyowahamasisha wanawake wenzako katika kujipatia kipato na kujijengea uwezo wa kiuchumi katika ngazi ya familia na taifa.

Blogu hii inaomba wanawake na wanaume wazidi kuwahamasisha wanawake wawezi kuwa wajasiriamali si wadogo tu bali kuwa pia wajasiriamali wakubwa na ikiwezekana kuwa na viwanda kuunga mkono kauli mbiu ya NCHI YA VIWANDA.

Blogu hii pia inawaomba watunga sera waweze kuwasaidia wanawake nchini kwa kuwa na sera nzuri za ujasiriamali kwa wanawake. Blogu hii pia inaomba suala la mafunzo kwa wanawake wajasiriamali litiliwe mkazo sana hasa kupitia kwenye vyuo vya ufundi (VETA) na Blogu hii inaamini kama mwanamke atakuwa na uwezo wa kiuchumi nchi yetu itasonga mbele na kuwa na maendeleo ya uhakika.
No comments:
Post a Comment