Tuwaenzi wazee wetu. Hongera Mh Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kuwakumbuka wazee wetu hasa waliopigania taifa letu. Blogu hii imejisikia faraja baada ya kuona ukiwa na Mama Maria Nyerere. Mama Maria ni mmoja wa wazee wetu mashuhuri. Blogu hii inaomba ukiwa kama Waziri unayeshughulikia pia masuala ya wazee uendelee kuwapa kipaumbele wazee wetu hasa katika masuala ya afya na matibabu kisera na kimkakati. Blogu hii inatambua kuwa wazee wengi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo maradhi yanayotokana na umri mkubwa.

No comments:
Post a Comment