Friday, May 5, 2017

Hongera Makamu wa Rais Mama Samia kwa kuwapa kipaumbele makandarasi wa ndani

Image may contain: 1 person, closeup
Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza na wakandarasi wa ndani jana (04 MEI 2017) amesema serikali itawapa kipaumbele wakandarasi wa ndani. Hakika tamko hili limekuja wakati muafaka ambapo itainua kipato cha wakandarasi wa ndani na kuinua uchumi wa nchi.

Blogu hii inaomba wakandarasi wa ndani wafanye mambo yafuatayo:
  • Kufanya kazi kwa weledi na uaminifu mkubwa;
  • Kukamilisha kandarasi kwa viwango kwa mujibu wa mikataba;
  • Kukamilisha kandarasi kwa wakati na kwa mujibu wa mikataba;
  • Kujiunga pamoja na kushirikiana katika kazi ili kushindana na wakandarasi wa nje wenye nguvu.
Tokeo la picha la samia suluhu hassan

Aidha, blogu hii inaiomba serikali kuweka sera ambazo zitawawezesha makandarasi wa ndani kupata kiurahisi mikopo ya vifaa na kifedha.

No comments:

Post a Comment