Hongera Mbao FC toka jijini Mwanza (the rock city) kwa kuingia FAINALI ya kombe la AZAM FA Cup baada ya kuifunga timu kongwe ya YANGA ya jijini Dar es Salaam. Mbao FC imekuwa chachu kwa timu nyingine ndogo ukiondoa vilabu vya YANGA, SIMBA na AZAM.
Blogu hii inaomba timu hii isibweteke na kuhakikisha inachukua kombe ili kuweka historia mpya nchini. Aidha vilabu vingine vidogo viige mfano wa Mbao FC. Blogu hii inaamini moja ya mafanikio ya Mbao ni kuwa na benchi zuri la ufundi, uongozi mzuri pamoja na wachezaji wenye vipaji na nidhamu ya mchezo. Ni muhimu kwa vilabu nchini Tanzania kuwa na vitu hivi muhimu kama Mbao FC. Hongera Mbao FC ya jijini Mwanza.
No comments:
Post a Comment