Sunday, December 13, 2015

Hongera Mawaziri na Manaibu Waziri kwa kuteuliwa na Mh Rais Dr MAGUFULI

Rais John Magufuli akisalimiana kwa furaha na wanahabari mara baada ya kutangaza baraza lake la mawaziri, Ikulu Dar es Salaam jana. (Picha na Ikulu).
Picha: Rais Magufuli akisalimiana na wanahabari baada ya kutangaza Baraza jipya la Mawaziri Ikulu jijini Dar es Salaam
 (source:habarileo)

Hongera baadhi ya watanzania wachache mlioteuliwa na Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kuwa Mawaziri na Manaibu Waziri wa Wizara mbalimbali. Hakika Mh Rais kawaamini sana na ana matarajio makubwa kuwa mtatenda kazi kwa uaminifu, uadilifu, na uweledi wa hali ya juu. Vile vile wananchi wa Tanzania wana matarajio makubwa na nyinyi wateule ukizingatia kasi nzuri ya Mh Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Jumamosi ya tarehe 12/12/2015 wataule mmeapishwa kwa kura kiapo. Kiapo kina maana kubwa sana kwenu binafsi, kwa Rais na kwa wananchi wa Tanzania. Blogu hii inamwomba Mwenyezi Mungu awaongoze katika utendaji wenu. Wananchi wengi wamefurahia uteuzi wenu kama inavyoonekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari, mfano habari leo.

Blogu hii inawapongeza sana kwa kuteuliwa na inawaomba mchape kazi usiku na mchana ili Tanzania isonge mbele kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa mtu mmoja mmoja na kwa taifa kwa jumla. 

Thursday, December 10, 2015

Asante Rais DKT John Pombe Magufuli kwa kufanya usafi na kuwaongoza watanzania kwa vitendo siku ya Uhuru 9 Disemba 2015


Picha: Jana tarehe 9 Disemba 2015, Mh Rais DKT John Magufuli akifanya usafi maeneo ya Ferry jijini DSM

Hongera Mheshimiwa DKT John Pombe Magufuli kwa kuwaongoza watanzania kwa vitendo kwenye siku ya Uhuru jana tarehe 9 Disemba 2015. Hakika blogu hii imefurahishwa na agizo la kutumia sherehe za Uhuru kufanya usafi nchini na pia kwa wewe binafsi kushiriki kufanya usafi ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa kuzoa uchafu kwa kushirikiana na wananchi wa kawaida.

Kuongoza kwa vitendo sio tu kumeweza kumewahamasisha wananchi kushiriki kwenye shughuli zao za maendeleo na za kijamii bali kumewakumbusha viongozi wengine kuwa "uongozi" ni kuonyesha "njia", na wewe umeonyesha kwa njia kwa vitendo. Blogu hii inasema ASANTE, na endelea kwa kasi hiyo hiyo.

Pia blogu hii inaziomba taasisi kama NEMC, Majiji, Manispaa, na Halmashauri za Miji na Wilaya kuhakikisha zinakuwa na "mipango endelevu" ya "usafi na utunzaji mazingira", kwa kila siku. Kwa mfano, Manispaa zinaweza kuwatumia wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe wake kutekeleza mipango ya usafi na utunzaji wa mazingira. 

Pia Manispaa zinatakiwa kwenda mbali zaidi kwa kuwatumia mabwana na mabibi afya wake kuhakikisha maeneo yote nchini iwe kwenye mahoteli, baa, mashule, vyuo, taasisi za umma na binafsi, mitaani na barabarani kwa uchache  kunakuwa na usafi na utunzaji wa mazingira unaostahili. Pia kuwe na ufuatiliaji kwa watakaokuwa wanachafua mazingira na kutupa uchafu ovyo, adhabu kali zitolewa. Lakini kuwe na "incentive" au motisha kwa taasisi au watu watakaokuwa mfano bora wa utunzaji mazingira na usafi, na tuzo hizi ikibidi ziwe mpaka ngazi ya wilaya, vitongoji na vijiji. Hakika usafi na mazingira bora, Tanzania INAWEZEKANA

Mwenyezi Mungu azidi kukupa nguvu RAIS wetu ili uweze kuwafikisha watanzania mahala panapostahili. Hakika Uhuru ni KAZI!!!

Thursday, November 19, 2015

Hongera Mh. Majaliwa kwa kupendekezwa na Rais kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania

Picha:pmoralg.go.tz

Hongera Mh. Kassim Majaliwa kwa kupendekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Blogu hii haina shaka na utendaji na uzoefu wako serikalini na hasa ulipokuwa TAMISEMI. Aidha blogu hii inatambua umakini, hekima, busara na upole ulionao. Kwa sasa blogu hii inakupongeza na kukutakia kila la kheri wakati Bunge likisubiriwa kukupitisha.

Wednesday, November 18, 2015

Hongera Mh Ndugai kwa kuchaguliwa kuwa Spika mpya wa Bunge la Tanzania 2015 - 2020

Picha: Habarileo.co.tz

Hongera Mh Job Ndugai kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Spika mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha 2015 - 2020. Ushindi huo unathibitisha imani kubwa walionayo wabunge katika kusimamia chombo hiki muhimu kwa ustawi wa nchi yetu. Ni imani ya blogu hii utatimiza majukumu yako ikiwemo kuishauri na kuisimamia serikali ili Tanzania ipige hatua kubwa ya maendeleo. Hongera sana Mh Ndugai, Mwenyezi MUNGU akuongoze ili uliongoze Bunge hili kwa hekima, amani na upendo kwa kuzingatia kanuni, sheria na katiba.

Saturday, November 7, 2015

Tanzania isimamie AHADI 10 za mwana TANU kwa ukamilifu ili tupate taifa ADILIFU na lenye kuleta maendeleo kwa WOTE

Kwanza kabisa isieleweke vibaya kunukuu AHADI za mwana TANU. Blogu hii imeona AHADI za mwana TANU kama zikitumika nchi yetu itasonga mbele kwa kasi kubwa sana. TANU ni chama kilicholeta ukombozi toka kwa wakoloni. Kila mwananchi alipenda siasa hii chini ya usimamizi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa sababu ilijali utu wa binadamu, ilikuwa ikiwainua wanyonge na ililenga kulijenga Taifa katika misingi ya haki na usawa. Aidha mwananchi yoyote bila ya kujali hadhi yake alipotakiwa kujiunga na chama hizi ndizo ahadi kumi alizotakiwa kuzitekeleza kwa vitendo kinyume cha hapo hatua kali zinachukuliwa. Ahadi kumi za mwana TANU zilikuwa kama ifuatavyo:

  1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.
  2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote.
  3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
  4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.
  5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
  6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.
  7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.
  8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
  9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanganyika (sasa Tanzania) na Afrika.
  10. Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanganyika (sasa Tanzania).

NAOMBA KILA MTU ASOME AHADI HIZI MWOYONI MWAKE NA AJIULIZE AMETEKELEZA NGAPI?

Blogu hii inamuomba rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania DKT John Pombe Joseph Magufuli na serikali yake atekeleze AHADI za mwana TANU. Blogu hii inatamani sana AHADI hizi zirudi na zitumike na kila mwana wa nchi hii bila kujali dini, kabila, elimu, kipato, chama, jinsi yake. Ahadi hizi zifundishwe toka shule za awali mpaka chuo kikuu ili tuzalishe taifa lenye UADILIFU uliotukuka. Naomba viongozi wote wa ngazi zote na hasa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ahakikishe AHADI hizi zinaimbwa na kila mtoto na mtu mzima wa taifa hili, zinatekelezwa na kila mtoto na mtu mzima wa taifa hili na pale zinapokiukwa HATUA kali zichukuliwe. Kwa kutizima AHADI hizi Tanzania itakuwa nchi bora sana. 

Thursday, November 5, 2015

Asante WATANZANIA kwa kudumisha AMANI wakati na baada ya UCHAGUZI

Picha:tanzaniatoday.co.tz

Asante WATANZANIA kwa kudumisha AMANI wakati na baada ya UCHAGUZI wa rais, wabunge na madiwani nchini Tanzania. Hakika Tanzania ni kisiwa cha AMANI. Blogu hii inawakumbusha watanzania wazidi kudumisha AMANI mara baada ya Rais wa AWAMU ya 5 kuapishwa. Blogu hii inasisitiza Mh. DKT. John Pombe MAGUFULI ni Rais wa WATANZANIA wote.

Hongera Mh MAGUFULI kwa kuapishwa na kuwa Rais wa TANZANIA

Picha:taarifa.co.tz

Hongera Mh. DKT. John Pombe MAGUFULI kwa kuapishwa na kuwa Rais wa awamu ya 5 ya Tanzania. Leo alhamisi tarehe 05 Novemba 2015 ni siku ya kukumbukwa na watanzania mara baada ya kuapishwa kama Rais wa Tanzania. Hakika watanzania wamekuamini na wanakutegemea katika kuwaletea maendeleo ya kweli. Ni matumaini ya Blogu hii kuwa utawaletea watanzania maendeleo kwa kasi kubwa. Blogu hii inaamini imepata mtetezi wa wanyonge. Mwenyezi MUNGU akubariki na kukulinda katika kuwatumikia wananchi wote.

Aidha Blogu hii inawaomba watanzania wote waunganishe NGUVU katika kuhakikisha ahadi za MAGUFULI na CCM zinatekelezwa kikamilifu. 

Hongera KIKWETE kwa kumaliza uongozi salama kama Rais

Picha: taarifa.co.tz

Hongera Mh. DKT. JAKAYA KIKWETE kwa kumaliza uongozi salama kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Leo tarehe 05 Novemba 2015 katika uwanja wa UHURU jijini Dar es Salaam umemkabidhi kijiti cha uongozi Mh John Pombe Magufuli. Kwa kiasi kikubwa umejitahidi kuwatumikia wananchi. Blogu hii inasema ASANTE na upate mapunziko MEMA.

Friday, October 30, 2015

Hongera Ms NATU MSUYA kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa BODI ya Wadhamini wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF)

Katika Picha: Ms Natu MSUYA kwenye picha ya pamoja na ujumbe toka Chuo cha NENU 
uchina ukiongozwa na Vice President Prof Gao Hang wa NENU pamoja na ujumbe wa DUCE ukiongozwa na 
Prof Joseph Buchweishaija, Makamu Mkuu wa Chuo/Utawala DUCE kwa ajili ya mazungumzo ya ushirikiano 24 Oktoba 2015

Hongera Ms NATU MSUYA kwa kuteuliwa na mamlaka husika kuwa Mwenyekiti wa BODI ya Wadhamini wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF). Blogu hii inatambua uwezo, weledi na uaminifu wako katika kazi mbalimbali ulizokuwa unafanya na unazofanya mpaka sasa. Blogu hii inaamini uwezo, weledi na uaminifu wako katika kazi utakuwezesha kufanya kazi vyema katika BODI hiyo. Mungu akulinde katika majukumu uliyopewa kwa taifa. Blogu hii inawashukuru wafuatao ambao kwa namna moja ama nyingine wamewezesha wewe NATU kufanya kazi kwa bidii na kuonekana na taifa kama vile Prof Rwekaza Mukandala (Makamu Mkuu wa UDSM), Prof William Anangisye (Mkuu wa chuo DUCE) na Prof Joseph Buchweishaija (Makamu Mkuu wa Chuo-Utawala/DUCE).

Hongera Mh MAGUFULI kwa kuchaguliwa na wananchi wa Tanzania kwa kura nyingi

Picha: africanleadership.co.uk

Hongera Mh John Pombe MAGUFULI kwa kuchaguliwa na wananchi wa Tanzania kwa kura nyingi. Hakika watanzania wamekuamini na kukupa kura kwa matarajio makubwa sana. Ni matumaini ya Blogu hii kuwa utawaletea watanzania wote maendeleo ya dhati. Hakika Blogu hii inaamini imepata si tu RAIS bali mlinzi na mtetezi wa wanyonge. Mwenyezi MUNGU akubariki na kukulinda.

Aidha Blogu hii inawakumbusha watanzania kuwa katika uchaguzi kunakuwa na ushindani mkubwa wa pande mbalimbali zinazotaka kuongoza nchi LAKINI akishapatikana MSHINDI ni jukumu la wote kushirikiana kuijenga nchi kwa UAMINIFU na WELEDI mkubwa.

Thursday, September 24, 2015

Nchi hii inahitaji mtu kama huyu (Nehemiah Mchechu Mkurugenzi wa NHC)

Hongera Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia kwa Mkurugenzi wake Mkuu Ndugu Nehemiah Kyando Mchechu kwa ujenzi wa makazi bora kabisa nchini. Hakika nchi hii inahitaji watu wenye akili, ujasiri na uthubutu kama wewe. Blogu hii inakutakia kila la kheri wewe na manejimenti nzima ya NHC katika ujenzi wa makazi bora. Ombi la blogu hii ni kuomba kwa kadri itakavyowezekana zijengwe nyumba za bei nafuu kwa wananchi wa kawaida. Na pia NHC iangalie uwezekano wa kuwakopesha watumishi wa umma nyumba kwa mikopo ya muda mrefu kama miaka 30+.


Monday, September 14, 2015

Hongera JK kwa kuzindua Taasisi ya MOYO ya Jakaya Kikwete

Picha: Habari leo
Hongera Mh. Dkt. Jakaya Kikwete kwa kuzindua Taasisi ya MOYO ya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam. Kupitia Taasisi hii Serikali itakuwa ikiokoa TShs Bilioni 2.5 kwa mwaka kutokana na upelekaji wa wagonjwa nje ya nchi.

Blogu hii inampongeza sana JK na serikali kwa ujumla kupitia wizara ya afya kwa uzinduzi wa taasisi hii ya kisasa ya magonjwa ya moyo katika ukanda wa Afrika Mashariki. Blogu hii inaomba jengo na vitendea kazi vitunzwe ili lengo la serikali likamilike. Aidha blogu hii inaishukuru serikali ya China kwa kutoa msaada wa Tshs Bilioni 16.6 katika ujenzi wa jengo la taasisi hii kutokana na jitihada zilizofanywa na Rais Kikwete alipotembelea China na kukutana na Rais Hu Jintao.

Hongera JK kwa kuzindua kampeni ya kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia UTALII

Picha: Wizara ya Maliasili na Utalii
Hongera Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuzindua kampeni maalum ya kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia mtandao na kampeni ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini. Blogu hii inampongeza sana Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyarandu pamoja na Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii Dkt, Adelhelm Meru na Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Taifa ya Utalii. Bi. Devota Mdachi kwa kuandaa mtazamo mpya wa kutangaza vivutio vya Utalii kimataifa.
Uzinduzi huo ulifanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali, wadau wa uhifadhi pamoja na wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Katika mpango huo vivutio vya utalii vitaonekana katika vituo vya kimataifa kama BBC, CNN nk na hii itachochea sekta ya Utalii nchini.
Blogu hii inaishukuru sana serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuandaa mpango wa kutangaza vivutio vya UTALII nchini. Blogu hii inaomba yafuatayo:

  1. Kuendelea kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia vyombo vya habari vingine hasa majarida na magazeti ya kimataifa;
  2. Kutangaza vivutio kwa watanzania kupitia televisioni za hapa nchini na magazeti ya kila siku (tusisahau utalii kwa watu wa ndani);
  3. Kuimarisha miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege nk ili kuchochea utalii nchini.
Kwa habari zaidi bofya hapa.

Hongera Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuahidi kushirikiana na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu ya Utalii nchini

Picha:Wizara ya Maliasili na Utalii

Hongera Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuahidi kushirikiana na sekta binafsi katika kuboresha miundombinu ya Utalii nchini kwa kusudi ya kuwavutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vingi vya utalii vilivyopo Tanzania. Miundombinu kama barabara zimekuwa katika hali mbaya na kukwamisha jitihada za serikali kuongeza watalii nchini.

Akizungumza katika mkutano wa sita wa Uchumi wa Tanzania ulioandaliwa na Benki ya Dunia katika Hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa Tanzania Mh Benjamini Mkapa alisema ni lazima sekta binafsi ishirikiane na Serikali badala ya Serikali kufanya kila kitu. SERIKALI HAIWEZI KUFANYA KILA KITU HIVYO SEKTA BINAFSI LAZIMA ISHIRIKISHWE KATIKA KUINUA UCHUMI.

Blogu hii imefurahishwa na Wizara ya Maliasili na Utalii ya kukubali kushirikiana na sekta binafsi katika kukuza sekta hii muhimu nchini kwa ustawi wa taifa letu. Pia blogu hii inawaomba watanzania na hasa wawekezaji wa ndani kuchangamkia fursa hii ili kujipatia kipato na kuinua pato la taifa.

Kwa habari zaidi, bofya hapa.

Saturday, September 12, 2015

Hongera Taifa stars kwa kuionyesha dunia kuwa mnaweza


Picha: Mwananchi.co.tz

Hongera Taifa stars kwa kuonyesha dunia kuwa mnaweza katika mechi kati ya Tanzania "Taifa stars" na Nigeria "Green Eagles" iliyochezwa jijini Dar es Salaam. Mechi hiyo iliyochezwa Septemba 5 2015 kuwania tiketi ya kufuzu AFCON 2017. Hakika wachezaji wamecheza kwa bidii sana wakiongozwa na Mbwana Samatta na Haji Mwinyi. Hakika kila mchezaji ameonyesha kiwango kikubwa. Haikuwa rahisi kuona tofauti ya kiuchezaji kati ya wachezaji wa kulipwa wa Nigeria na wale wanaocheza ligi ya ndani ya Tanzania. Benchi la ufundi nalo linastahili pongezi za dhati likiongozwa na Charles Boniface Mkwassa aka "Master" na Abdallah "King" Kibadeni aka "Mputa". Aidha blogu hii inaipongeza TFF kwa jitihada ilizofanya za kuibadili timu hii. Blogu hii inaomba juhudi hizo ziendelezwe. Pia blogu hii inaiomba serikali izidi kushirikiana na TFF katika kuisaidia timu ya Taifa. 

Tuesday, August 18, 2015

Hongera DART na Wizara ya Ujenzi kwa kufanikisha mradi wa mabasi yaendayo haraka. Tuache tabia mbaya


Hongera DART, wizara ya Ujenzi na Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kufanikisha mradi wa mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (Dar es Salaam Bus Rapid Transit - BR) toka Kimara kwenda Kivukoni. Kiujenzi, mradi huo umetekelezwa na Strabag International GmbH. Haya wakazi wa Dar es Salaam usafiri mzuri ndio huo. Tuwe wastaarabu. Tuache lugha mbaya kama abiria, dereva na konda. Pia mamlaka husika izingatie usafi na utunzaji wa mabasi haya.Usafiri huu ni kama wa nchi zilizoendela ambapo kuna teknolojia ya mawasiliano ambapo abiria, dereva na konda watakuwa wakichunguzwa muda wote.

Blogu hii inaomba mamlaka husika kuyatunza mabasi haya na kuhakikisha kila anayevunja sheria adhabu kali inatolewa bila huruma.

Wednesday, August 12, 2015

Hongera UKAWA kwa kufanya maandamano makubwa yenye utulivu na amani nchini

Hongera UKAWA kwa kufanya maandamano yenye utulivu na amani. Tarehe 10/08/2015 itakuwa siku ya kukumbukwa hapa nchini Tanzania baada ya mgombea wa urais kwa tiketi ya Chadema kupitia UKAWA. Hakika blogu hii imefurahishwa na utulivu na amani ulioonyeshwa kupitia maandamano haya makubwa nchini. Maandamano haya yalikuwa ya kumsindikiza Mh Edward Lowassa kuchukua fomu za kugombea urais katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Blogu hii inaomba vyama vingine pamoja na wadau wengine kudumisha amani.

Thursday, August 6, 2015

Hongera JK kwa kuwajali wasanii nchini

Picha:blog.ikulu.go.tz
Hongera Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete "JK" kwa kuwajali na kuwathamini wasanii nchini Tanzania. Sekta ya usanii hapo zamani ilikuwa inaonekana ni sekta ya kibabaishaji, lakini sasa imekuwa sekta rasmi inayochangia uchumi wa nchi yetu. JK umejitahidi kuwainua na kuwatambua wasanii wetu. Tunaomba Rais ajaye afuate nyayo zako ili sekta hii itoe mchango mkubwa kwa uchumi wa taifa letu. 

Blogu hii imefurahishwa sana kwa Rais kujumuika na wasanii siku ya alhamisi tarehe 6 mwezi wa 8 mwaka 2015. JK umekuwa shujaa wa wasanii nchini. Asante wasanii kwa kazi njema za kuwaburudisha watanzania, asante NIKI WA PILI kwa hotuba yako nzuri, hakika uko juu sana. Asante JK kwa kukubali kuwa mlezi wa wasanii.

Blogu hii inaomba serikali kuweka mikakati dhabiti katika ulinzi wa biashara za wasanii na ulinzi wa maisha ya msanii mmoja mmoja na haki zao. Mfano, wasanii wanaweza kuingizwa kwenye bima za afya na bima nyinginezo kupitia "shows" zao. Na hii inawezekana, serikali ijayo ifanye hayo.

Sunday, August 2, 2015

Hongera Azam FC kwa kuchukua kombe la KAGAME 2015

Picha:en.wikipedia.org
Hongera Azam FC kwa kuchukua ubingwa, Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki lijulikanalo kama "Kombe la Kagame" Jumapili (02/08/2015) kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Ushindi wa Goli 2 - 0 dhidi ya Gor Mahia ya Kenya ni mkubwa na umewafurahisha sana watanzania na kuwaondolea unyonge. Blogu hii imefurahishwa na juhudi ya timu hii pamoja na benchi lake la ufundi na manejimenti kwa ujumla. Jambo zuri sana ni kuwa timu hii katika mashindano haya haijafungwa goli lolote ndani ya dakika dk 90 katika michezo yake yote.

Hakika kikosi hiki kilichochukua ubingwa hakita sahaulika:


  1. Aishi Manula
  2. Shomari Kapombe
  3. Said Morrad
  4. Aggrey Morris
  5. Serge Wawa
  6. Mugiraneza Jean Baptiste
  7. Himid Mao
  8. Kipre Tchetche/Kavumbagu
  9. Ame Ally/Frank Domayo
  10. John Bocco
  11. Farid Mussa/ Erasto Nyoni
Blogu hii inajua kuwa timu ya Azam FC ina mfumo mzuri, ina uwanja wake, ina vifaa vya michezo vya uhakika, inalea vijana wadogo nk. Vitu hivi ndio chachu kubwa ya ubingwa wao wa Kagame. Blogu hii inaomba juhudi hizi za Azam FC ziendelee hata kwenye kombe la washindi barani Afrika ili jina la Tanzania lizidi kupaa.Hakuna kama Azam FC Tanzania!!

Kwa habari zaidi tembelea Azam FC

Monday, July 20, 2015

Hongera sana Diamond Platnumz kwa ushindi ulioupata barani Afrika 2015

Picha:en.wikipedia.org

Hongera sana Diamond Platnumz kwa ushindi ulioupata barani Afrika. Katika Tuzo zilizotolewa na kituo cha Television cha MTV nchini Afrika Kusini, msanii wa Tanzania Diamond ameshida kwa kishindo tuzo ya mtumbuizaji bora barani Afrika "Best Live Act" kupitia shindano la MTV (MAMA'S) Africa Music Awards 2015. Shindano hilo lilifanyika ndani ya ukumbi Durban International Convention Center (ICC) nchini Afrika Kusini 19 Julai 2015.

Blogu hii imefurahishwa na ushindi wa msanii huyu wa Tanzania na imemwomba azidi kupambana na kupiga hatua zaidi kimataifa. Pia blogu hii inawaomba wasanii wengine wa Tanzania kuiga na kufuata nyayo za Diamond ili wapate mafanikio. Blogu hii inaomba watanzania wakiwemo wadau wote wa muziki nchini kuwa wakweli katika upatikanaji wa washindi katika tuzo mbalimbali ili kusaidia kuibua na kukuza vipaji na sio kuvidumaza. 

Hakunaga kama Diamond Platnumz.

Wednesday, July 15, 2015

Hongera Azam TV kwa kuwa na mpango wa kuonyesha ligi kuu ya Hispania "La Liga" mwaka huu


Picha:sundayshomari.com

Hongera Azam TV kwa kuwa na mpango wa kuonyesha ligi kuu ya Hispania "La Liga" mwezi wa 8 mwaka 2015. Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Uhai Production Dunstan Tido Mhando jana tarehe 14 mwezi wa 7 mwaka huu kupitia Azam two ya Azam TV. Blogu hii imefurahishwa na hatua nzuri ambayo itatoa burudani kabambe kwa wana wa Afrika Mashariki na hasa wapenzi wa soka. 

Ni matarajio ya blogu hii kuwa kuwepo na maonyesho ya ligi kubwa duniani kutaenda sambamba na unafuu wa bei ili kuwawezesha watu wengi kuona burudani hii majumbani mwao.

Blogu hii inawaomba watu wazidi kujiunga na Azam TV ili izidi kutupa burudani na habari kwa uhakika na kwa bei nafuu. Hakika hakuna kama Azam TV katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Monday, July 13, 2015

Hongera Mh Samia Suluhu Hassan kwa kuteuliwa kuwa Mgombea Mwenza kupitia CCM

Picha:tanzaniatoday.co.tz

Hakika wanawake wanaweza! Hongera Mh Samia Suluhu Hassan kwa kuteuliwa kuwa Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kuchaguliwa kwako kumeonyesha kuwa wanawake wanaweza kuongoza ngazi yoyote ya uongozi nchini Tanzania. Jana jumapili ya tarehe 12 mwezi wa 07 mwaka 2015 mjini Dodoma ilikuwa siku ya kukumbukwa na watanzania na hasa wakinamama nchini.

Kitendo hiki kimetoa hamasa kubwa kwa wanawake wengi nchini Tanzania kujiamini kuwa wanaweza. Blogu hii inaomba wanawake wazidi kujitokeza katika kuwania nafasi za maamuzi na kisiasa nchini Tanzania kupitia uchaguzi mkuu utakaofanyia oktoba mwaka huu 2015.


Hakika wanawake wanaweza!

Hakika wanawake wanaweza! Hongera Balozi Amina na Dr Asha-Rose

Picha: un.org

Hakika wanawake wanaweza! Hongera Balozi Amina Salum Ali na Dr Asha-Rose Mtengeti Migiro kwa kuonyesha kuwa wanawake wanaweza. Kufika kwenu kwenye TATU BORA ya kutafuta mgombea urasi kwa tiketi ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumeonyesha kweli na kwa hakika wanawake nchini Tanzania wana uwezo mkubwa sana katika ngazi za maamuzi. Wakina mama hawa walifika tatu bora jumamosi tarehe 11/07/2015 mjini Dodoma pamoja na Mh John Pombe Magufuli.

Tendo mlilofanya limetoa hamasa kwa wanawake wengine nchini kujiamini. Ni matarajio ya blogu hii kuwa kwa kufuata nyayo za wakina mama hawa (Balozi Amina Salum Ali na Dr Asha-Rose Mtengeti Migiro), wanawake wengi sana nchini watajitokeza katika kuomba nafasi za udiwani, ubunge na uwakilishi kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2015. Blogu hii inaamini, ili taifa hili liwe na ustawi unaostahili wanawake wanapaswa kushiriki kikamilifu katika ngazi za maamuzi na kisiasa.

Ombi la blogu hii ni kwa wapiga kura wanawake na wanaume kuwapigia kura za ndio MAMA zetu. Hakika NANI KAMA MAMA. HAKUNA.....

Picha:cctv-africa

Hongera John Pombe Magufuli, wewe ni JEMBE

Image result for magufuli
Picha:thehabari.com
Hongera John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kuipeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa Rais Oktoba 2015. Kura nyingi (asilimia 87.1) ulizopata ni ishara tosha ya kukubalika ndani ya CCM. Blogu hii imefurahishwa na ushindi wako mkubwa. Ushindi mkubwa uliopata ni kielelezo cha rekodi zako za utendaji ulio tukuka katika kuliletea taifa letu maendeleo. Blogu hii inaona sasa Tanzania inaelekea kuwa nchi yenye kipato cha kati duniani kama utachaguliwa na watanzania.

Blogu hii inatarajia vyama vingine navyo vitachaguwa watu wenye rekodi nzuri kama walivyofanya CCM katika uchaguzi wa Rais wa mwaka huu. 

Blogu hii inatarajia chini ya uongozi wako, nchi yetu itakuwa na barabara nyingi na zenye kiwango cha hali ya juu na kupunguza misongamano isiyo ya lazima; viwanja bora vya ndege vyenye hadhi ya kimataifa; bandari bora kama vile Dar es Salaam, Tanga, Bagamoyo na Mtwara; huduma bora za afya na elimu; matumizi bora ya ardhi ili kuondoa migogoro ya wakulima na wafungaji pamoja na kuondoa makazi holela; huduma bora za utalii pamoja na usafi wa miji na mazingira yetu kupitia halmashauri za miji na mikoa.

Blogu hii inaamini utatilia mkazo sekta mama ambayo ni ELIMU kwa maana sekta zote zinategemea ELIMU katika ujenzi wa taifa. Mkazo utakuwa kwenye kila janja ya elimu kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu. Aidha katika jambo linalosahaulika sana ni kuwa nchi hii inahitaji wahitimu wengi toka kwenye vyuo vya ufundi (vocational and technical education). Vijana kutoka eneo hili ndio tegemeo la taifa lolote kiuchumi.

Aidha blogu hii inatarajia suala la uwajibikaji na uadilifu kwa watumishi wote wa umma na viongozi litatiliwa mkazo unaostahili.

Thursday, July 2, 2015

Kama Ghana wameweza kutengeneza Gari na sisi Tanzania tunaweza! Tuwekeze kwenye utafiti na ubunifu

Picha: bbcswahili

Kama Ghana wameweza na sisi Tanzania tutaweza. Ghana ni mojawapo ya nchi ya Afrika na inayoendelea kama Tanzania, imeweza kutengeneza gari lake liitwalo "Kantanka" kama zilivyo nchi zilizoendelea kama Japan, Marekani, China, Australia na nyinginezo. Hakika hii ni hatua kubwa sana barani Afrika. Kwa watanzania na hasa kwa watunga sera na wasimamizi wa sera wakiwemo wataalamu toka vyuo vikuu na vyuo vya ufundi wakae na kuhakikisha Tanzania kupitia teknolojia inatangeneza magari na machine mbali mbali ambazo zitatumika ndani na nje ya nchi. Kama nchi tuwekeze kwenye utafiti na ubunifu zaidi.Kwa habari zaidi bofya hapa


Sunday, June 28, 2015

Hongera Mkwasa kwa kuteuliwa kuwa Kocha wa Taifa Stars

Image result for mkwasa
Picha: bbc.com
Hongera Charles Boniface Mkwasa kwa kuteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa "Taifa Stars". Hakika uteuzi huu umekuja wakati muafaka. Aidha blogu hii inapenda kuwapongeza wasaidizi wa Mkwasa kama vile Peter Manyika kocha wa makipa, Hussein Sued mtunza vifaa, Abdallah "King" Kibaden "Mputa" Mshauri Mkuu pamoja na Juma Mgunda Timu Meneja. Blogu hii inalipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini "TFF" kupitia kwa Rais wake Jamal Malinzi kwa kumteua na kumwamini kocha mzawa kuongoza timu ya taifa. Ni matarajio ya blogu hii kuwa Mkwasa na wenzake watapata ushirikiano mkubwa toka TFF kama ule waupatao makocha wa kigeni.

Blogu hii inaomba itoe iliyoyaona kabla ya Mkwasa kuchukua mikoba. Timu hii kabla ya Mkwasa kuingia ilikosa stamina, na kasi. Inawezekana kusimama kwa ligi Tanzania kukawa sababu. Pili, kuna wachezaji wamechoka na hawako makini. Tatu, inawezekana fomesheni inayotumika wachezaji hawailewi ivyo kutoa mwanya kwa timu pinzani kuinyanyasa timu yetu.

Ni matarajio ya blogu hii kuwa Mkwasa pamoja na benchi lake la ufundi wataweza kuwafuata machozi watanzania na kuifanya timu ya taifa iwe tishio Barani Afrika. Aidha ni matarajio yetu kuwa wachezaji nao watafuatilia maelekezo na mafunzo ya kocha kikamilifu huku wakizingatia nidhamu ya hali ya juu pamoja na kuwa wazalendo wa kweli kwa nchi yetu. Blogu hii inamwomba Mkwasa pamoja na wasaidizi wake wafanye kazi kikamilifu ili makocha wazawa nao waweze kuaminiwa na kuaminika.

Thursday, June 18, 2015

Hongera NMB kwa kuanzisha kadi za MasterCard

Hongera NMB kwa kuanzisha kadi za MasterCard. Kadi hizi zitawawezesha wateja wa Benki hii kutumia huduma za NMB popote duniani. Hakika haya ni mapinduzi makubwa kwa benki hii ambayo ni tegemeo kwa watanzania wengi.

Watanzania tujiunge na NMB kwa maendeleo yetu.

Kwa habari zaidi, tembelea NMB

mastercard

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Ndugu Mark Wiessing (katikati) 
na Makamu wa Rais wa MasterCard, Ukanda wa Sahara, 
Africa Ndugu Daniel Monehin wakisaini utoaji wa MasterCard 
milioni 1.5 hapa Tanzania. 
Chanzowww.nmbtz.com/


Tuesday, June 2, 2015

Hongera NSSF kwa kuanzisha mpango wa kuwakopesha wanachama kwa kupitia waajiri wao

Watanzania tujiunge na NSSF ili 
kuboresha MAISHA YETU!!

Image result for ramadhani dau

Hongera Shirika la Taifa la Mfuko wa Jamii (NSSF) kwa kuwajali wanachama na hasa watumishi wa umma na binafsi kwa kuanzisha mpango wa kuwakopesha pesa kupitia waajiri wao. Hakika mpango huu ni mzuri sana na utawakomboa wafanyakazi kimapato na kiuchumi. Haya yamesemwa leo tarehe 2 mwezi wa 6 mwaka 2015 jijini Arusha kwenye Mkutano wa Wadau na Wanachama wa NSSF nchini ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Pinda. 

Aidha NSSF imetenga kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuhamasisha ujasiriamali nchini. NSSF imetenga pesa si chini ya Bilioni 50 kwa ajili ya kuwakopesha wajasiriamali fedha ili kuinua biashara zao. 

Blogu hii inaomba mipango hiyo miwili ianze kazi ili kutoa nafuu kwa wananchi na hasa watumishi na wajasiriamali nchini. Blogu hii inaomba wananchi na hasa watumishi wa umma na binafsi kuchangamkia fursa hii. Pia blogu hii inaomba waajiri nao kuhakikisha watumishi wanapata taarifa sahihi kuhusu huduma hizi za NSSF.

Hongera Dr Ramadhani Dau pamoja na manajimenti yako kwa juhudi kubwa unazofanya katika ujenzi wa taifa hili. 

Blogu hii inakumbukumbu ya juhudi na miradi mingi mikubwa ambayo inajenga uchumi na ustawi wa nchi ikiwemo ujenzi wa Chuo Kikuu Dodoma,  Daraja la Kigamboni, Mradi wa Nyumba za Makazi Mtoni kijichi, Mradi wa Nyumba wa Dege Eco Village nk.

Tembelea NSSF kwa habari zaidi.


Saturday, April 4, 2015

Hongera Shirika la Reli Tanzania (TRL) kwa uzinduzi wa treni ya abiria toka Dar es Salaam kwenda Kigoma

Hongera Shirika la Reli Tanzania (TRL) kwa uzinduzi wa treni ya abiria toka Dar es Salaam kwenda Kigoma. Hakika treni hiyo ni nzuri na ya kisasa kwa dunia ya leo. Treni hii ni tofauti na treni za zamani zilizokuwepo nchini. Abiria akipanda treni hii anakuwa kama yuko nyumbani kwake maana anapata huduma za kisasa kama vile uwezekano wa kuendelea kutumia kompyuta, internet, kuchaji simu nk muda wote wa safari. Pia viti vya treni hii havimfanyi abiria kuchoka tofauti na viti vya zamani. Treni hii licha ya kuongeza wigo wa usafari wa abiria nchini pia unaokoa maisha ya watu kwa kuwa usafiri wa mabasi umekabiliwa na ajali ambazo baadhi ni uzembe wa binadamu.

Blogu hii inaomba abiria kuzingatia usafi na pia TRL kuwa wakali kwa yeyote atakayechafua mandhari ya treni hii bila sababu ya msingi. Blogu hii inaomba TRL wajiwekee "standards" za huduma kwa wateja kama vile kufanya ukarabati na marekebisho ya mara kwa mara ili treni hii ifanane kwa viwango na treni nyingine zilizoko Ulaya, Marekani na Asia. Pia TRL kuhakikisha kila abiria anayepanda treni hii anapata kiti ama chumba na kuondoa uwezekano wa kuwa na abiria wengi wasiokuwa na nafasi. Blogu hii inatarajia TRL kuwa na mkakati wa kuwa na treni zinazoenda kwa mwendo wa haraka yaani "Express" inayosimama vituo vichache sambamba na "ordinary" inayosimama vituo vingi zaidi.

Blogu hii inaipongeza sana TRL pamoja na Wizara ya Uchukuzi kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwasaidia wananchi hasa wa mkoa wa Kigoma ambao walikuwa wakikabiliwa na tatizo sugu la usafiri. Blogu hii inaomba safari hizi ziwe za kila siku toka Dar es Salaam kwenda Kigoma. Pia kuwe na safari za kila siku kwenda mikoa mingine ya Tanzania kuelekea Moshi na Mwanza. Kwa habari zaidi soma mwananchi.

Picha: mwananchi.co.tz

Saturday, March 28, 2015

Hongera JK kwa kuzindua treni ya kubeba mizigo toka Dar es Salaam kwenda nchi jirani

Uzinduzi wa treni ya mizigo toka Dar es Salaam kwenda nchi jirani hususan Rwanda ni jambo jema sana kwa ustawi wa nchi za maziwa makuu na ukanda wa Afrika Mashariki. Aidha uzinduzi wa treni ya mizigo mbali na kupunguza gharama kubwa za usafirishaji pia zitapunguza kwa kiasi kikubwa muda unaopotea njiani kutokana na vikwazo mbalimbali barabarani. Pia uzinduzi huu utapunguza usumbufu usiokuwa wa lazima.

Blogu hii inaipongeza sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Dr Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutimiza lengo muhimu sana kwa uchumi wa Tanzania na nchi jirani. Hakika haya ndiyo maendeleo wananchi wanayoyataka. 

Blogu hii inaomba serikali ijikite zaidi kuhakikisha kuna kuwa na usafiri wa treni kila siku kwa ajili ya kusafirisha mizigo na abiria toka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani. Usafiri wa treni duniani kote ni usafiri wenye usalama na gharama nafuu ukilinganisha na usafiri wa mabasi. Aidha blogu hii inaomba serikali iwekeze katika usafiri wa reli ndani ya majiji kama vile Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Tanga na Arusha ili kukabiliana na msongamano wa magari barabarani. 

Kwa habari zaidi tembelea wavuti

Rais Kagame akinyanyua bendera kuashiria uzinduzi wa Treni ya Mizigo 
toka Dar es Salaam kwenda Rwanda (http://www.wavuti.com)

Saturday, March 7, 2015

Hakuna kama Azam Tv nchini Tanzania.


Picha: tanzaniatoday.co.tz

Hakuna kama Azam Tv. Jana tarehe 06 mwezi 03 mwaka 2015 itakuwa siku ya kukumbukwa katika sekta ya habari ya nchini Tanzania mara baada ya kituo cha Azam Tv kuzindua studio mpya ya kisasa yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 31 (zaidi ya bilioni 56 za kitanzania). 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. Jakaya Kikwete ndiye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo na ndiye aliyekata utepe akiambatana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Dr Fenella Mukangara sambamba na viongozi na wafanyakazi wa Azam Tv Tabata Relini jijini Dar es salaam.

Hakika blogu hii inaipongeza sana Azam Tv hususan wamiliki na uongozi wake kwa ujumla kwa juhudi za dhati za kuboresha sekta ya habari nchini. Kituo hiki ambacho kina mwaka mmoja toka kianzishwe kimepiga hatua kubwa sana. Moja ya hatua kubwa ambayo kila mtanzania anaiona ni kuonyesha "live" ligi mbalimbali za michezo ikiwemo Ligi Kuu ya Vodacom. Blogu hii inaamini Azam Tv itakuwa na ubora kama vituo vingine vya kimataifa kama vile BBC, CNN SKY nk. SISI ni Azam Tv wewe je?

Asante Mh. Dr. Magufuli kwa kumfagilia Mh. Mbowe na kuonyesha kuwa siasa sio chuki bali ni maendeleo

Picha:mwananchi.co.tz

Asante sana mpiganaji, mchapakazi na mzalendo wa kweli Mh Dr. John Pombe Magufuli kwa kuwafundisha wananchi wa Tanzania kuwa siasa sio chuki wala ugomvi. Siasa ni kuwa na mitazamo tofauti yenye nia moja ya kuwaletea wananchi maendeleo na si vinginevyo. Mh Dr. Magufuli alimtaja kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe (Mbunge wa Hai) kuwa ni kiongozi anayefuatilia maendeleo ya watu wake bila ya kujali itikadi za kisiasa. Mh Dr. Magufuli aliyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara inayotoka Kwasadala kupitia Masama mpaka Machame hivi karibuni.

Blogu hii inampongeza sana Mh Dr. Magufuli kwa kauli yake nzuri inayoleta umoja na amani ya kweli kwa watanzania. Blogu hii inawaomba wanasiasa wengine kuiga mwenendo huu kwani mitazamo tofauti ya siasa sio nongwa! Tuepuke watu wanaopenda kuona taifa hili ama viongozi wa kisiasa wakikinzana bila sababu ya msingi.

Kwa habari zaidi soma mwananchi.


Monday, March 2, 2015

Asante Rais Jakaya Kikwete kwa kutoa kauli dhabiti "kama kuwa na kiungo cha albino ndio kupata utajiri basi albino wote duniani ndio wangekuwa na utajiri mkubwa kuliko wote"

Image result for kikwete
Picha:thehabari.com
Maneno hayo yamesemwa leo (02/03/2015) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete wakati akihutubia taifa. Hakika kauli hiyo inapaswa kuingia akilini kwa watu wote na hasa kwa wale wenye imani potofu juu ya walemavu wa ngozi. Rais kwa mshangao alisema “kama kuwa na kiungo cha albino ndio kupata utajiri basi albino wote ndio wangekuwa matajiri wakubwa duniani”. Alisisitiza kama ingekuwa kweli basi wahusika (albino) ndio wangekuwa na utajiri mkubwa kwa kuwa wao wenyewe wana viungo hivyo mwili mzima! 

Hivyo amewaomba watu wapuuze ujinga uliopo kuwa viungo vya watu wenye changamoto ya viungo (albino) vinaleta utajiri. Janga hili ni kubwa na la ajabu ambalo dunia inatutizama kwa jicho la kustaajabu. Kila mmoja wetu kwa nafasi aliyonayo apambane na janga hili kwa nguvu kubwa. 

Blogu hii inampongeza sana Rais kwa kauli yake hii na pia inaomba vyombo vya serikali kuchukua na kutumia kauli hii katika kuondoa fikra mbovu ya baadhi ya watu wenye kufikiri viungo vya albino vinaleta utajiri. Pia blogu hii inaomba vyombo vya dola kupambana na waovu hawa kwa kasi kubwa. Pili mahakama ziendeshe kesi za waovu hawa kwa kasi kubwa pia. Blogu hii inaomba taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za kiserikali pamoja na Bunge la Jamhuri ya Muungano kukemea mauaji haya ya wenzetu wenye changamoto ya ngozi. 

Blogu hii inaamini sekta ya elimu ina mchango mkubwa katika kuwaelimisha watu toka wakiwa wadogo mashuleni na vyuoni ili kuondokana na dhana hii mbovu vichwani mwa watu.

Mwisho, blogu hii inatarajia wanaharakati wa haki za binadamu kupambana na uovu huu mkubwa.
J

Saturday, February 28, 2015

Hongera Mh John Pombe Magufuli na Mh Mwigulu Mchemba kwa kutoa msaada kwa mama mwathirika wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi

Hakika blogu hii inawapongeza kwa dhati kwa namna mlivyomjali Mama wa mtoto aliyetekwa na kuuwawa kikatili . Mtoto (Yohana Bahati) huyo mwenye umri wa mwaka mmoja alikuwa mlemavu wa ngozi mwenye “albinism”. Mama wa mtoto huyo baada ya kujeruhiwa wakati akipambana na watu waliomteka na kumuua mwanae amelazwa katika hospitali ya Bugando, mjini Mwanza. Msaada wenu wa shilingi milioni moja sio mdogo. Blogu hii inawapongeza sana na inawaomba mzidi kuwasaidia watu maskini na wenye mahitaji maalum.


Pia blogu hii inaomba viongozi na wadau wengine wajitokeze kusaidia katika mapambano dhidi ya ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi. Pia blogu hii inaomba serikali kupitia vyombo vyake ifanye “operation” kama ilivyofanya Tanga wakati ikipambana na watu waliokuwa wanasadikiwa ni majambazi ama magaidi. Pia kuwepo na mahakama maalumu ya kushugulikia kesi za watu wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi.

Image result for mwigulu nchemba
Picha: sundayshomari.com

Image result for john magufuli
Pichathehabari.com